Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




2 Samweli 18:22 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

22 Kisha Ahimasi mwana wa Zadoki akamwambia Yoabu tena: “Si kitu; uniruhusu na mimi nimukimbilie yule Mwetiopia!” Yoabu akamwambia: “Mbona unataka kukimbia mwana wangu? Wewe hautapata zawadi yoyote kwa habari hizi!”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




2 Samweli 18:22
6 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Halafu Yoabu akamwambia mutu mumoja wa inchi ya Etiopia: “Wewe, uende umwelezee mufalme yale uliyoona.” Mwetiopia yule akainama kwa heshima mbele ya Yoabu, akaondoka mbio.


Ahimasi akamwambia: “Si kitu; nitakimbia.” Yoabu akamwambia: “Basi, kimbia.” Kisha Ahimasi akakimbia akifuata njia ya mbuga, akamutangulia yule Mwetiopia.


Mufalme akamwambia: “Kijana Abusaloma ni muzima?” Ahimasi akasema: “Wakati Yoabu aliponituma mimi mutumishi wako, niliona kulikuwa kelele nyingi, lakini sikufahamu maana yake.”


Lakini mufalme wa Misri akamwuliza: “Nimekunyima nini hata uamue sasa kurudi katika inchi yako?” Naye Hadadi akasema: “Uniache tu niende.”


Hivi kufuatana na vile walivyokataa kumutambua Mungu, Mungu akawaacha wafuate akili yao ya upotevu, kusudi wafanye mambo wasiyopaswa kufanya.


Vilevile kusisikilike maneno ya matusi ya ovyo ovyo wala machafu, kwa maana hayana mafaa. Kinachofaa ni kumushukuru Mungu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ