Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




2 Samweli 18:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Daudi akatuma waaskari wake kwa vita katika vikundi vitatu: sehemu moja ya tatu ikiwa chini ya uongozi wa Yoabu, sehemu ingine ya tatu chini ya uongozi wa Abisayi mwana wa Zeruya, ndugu ya Yoabu; na sehemu ingine ya tatu chini ya uongozi wa Itayi wa muji wa Gati. Kisha mufalme Daudi akawaambia wote: “Mimi mwenyewe vilevile nitakwenda pamoja nanyi.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




2 Samweli 18:2
14 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Shauri langu ni kwamba uwakusanye kwako watu wote wa Israeli tangia Dani mpaka Beri-Seba wakuwe wengi kama muchanga wa bahari, na wewe mwenyewe peke yako uende kwa vita.


Lakini Abisayi mwana wa Zeruya alikwenda kumusaidia Daudi. Abisayi alimushambulia yule Mufilistini na kumwua. Kwa hiyo, watu wakamwapia Daudi wakisema: “Hautakwenda tena nasi katika vita, kusudi usiizime taa ya ufalme katika Israeli.”


Abisayi mwana wa Zeruya na ndugu ya Yoabu alikuwa mukubwa wa mashujaa makumi tatu. Yeye alipigana kwa mukuki wake na watu mia tatu, akawaua, akajipatia sifa pamoja na wale mashujaa watatu.


Yoabu mwana wa Zeruya alikuwa jemadari wa makundi yake ya waaskari. Yosafati mwana wa Ahiludi alikuwa mwandishi wa habari za kifalme.


Yoabu alipopata habari, alikimbilia katika hema ya Mungu na kushikilia pembe za mazabahu kwa maana alikuwa amemwunga Adonia mukono ingawa mbele hakukuwa na Abusaloma.


Ninalala na kupata usingizi, ninaamuka tena, maana wewe ni tegemeo langu.


Basi akawagawanya wale watu mia tatu katika makundi matatu, akawapa baragumu na mitungi yenye mienge.


Ilipokaribia saa sita za usiku, Gideoni na kundi lake la watu mia moja wakafika kwa mwisho wa kambi, kwa mwanzo wa zamu ya kati. Wakati walipokuwa wamebadilisha wenye zamu, wakakaribia kambi ya waadui. Wakapiga baragumu na kuvunja mitungi waliyokuwa nayo.


Akatwaa watu wake akawagawanya katika vikundi vine, kusudi waende kuvizia katika mashamba. Alipowaona watu wanatoka katika muji, akatoka alikojificha akawaua.


Kesho yake, Saulo aliwagawanya watu katika vikundi vitatu. Wakati wa zamu ya asubui, wakaingia kwenye kambi ya adui, na kuwashambulia Waamoni. Kufikia saa sita za muchana waadui wengi walikuwa wameangamizwa. Wale waliobaki walitawanyika ovyo, hata hakukuwa kikundi chochote kati yao hata cha watu wawili tu pamoja.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ