2 Samweli 18:19 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
19 Kisha, Ahimasi mwana wa Zadoki, akasema: “Uniruhusu nikimbie kumupelekea mufalme habari hizi kwamba Yawe amemukomboa toka katika nguvu za waadui zake.”
Watoto wao wawili wanaume, Ahimasi mwana wa Zadoki na Yonatani mwana wa Abiatari, wako pamoja nao. Na neno lolote mutakalosikia mutanipasha habari kwa njia yao.”
Wakati ule, Yonatani na Ahimasi walikuwa wakimungojea karibu na Eni-Rogeli, kusudi wasionekane na mutu yeyote wakiingia katika muji. Kila mara mujakazi fulani alikuwa akiwapelekea habari nao wakaipeleka kwa mufalme Daudi.
Yoabu akamwambia: “Leo, hautapeleka habari hiyo. Unaweza kupeleka habari hizo siku nyingine. Lakini leo hautapeleka habari zozote kwa sababu mwana wa mufalme amekufa.”
Halafu yule Mwetiopia akafika; naye akasema: “Kuna habari njema kwako bwana wangu mufalme! Maana Yawe leo hii amekukomboa kutoka nguvu za wale wote waliokushambulia.”
Lakini wewe unawaona wenye taabu na shida; nawe uko tayari kuwasaidia siku zote. Muzaifu anakutegemea wewe, ee Mungu, wewe umekuwa siku zote musaada wa yatima.
Wandugu wapendwa, musilipize kisasi ninyi kwa ninyi, lakini mumwachie Mungu wakati wa kutenda kufuatana na kasirani, maana imeandikwa katika Maandiko Matakatifu: “Ni kazi yangu kulipiza kisasi. Ni mimi nitakayelipiza.”