Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




2 Samweli 18:18 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

18 Abusaloma, alipokuwa angali anaishi, alikuwa amejijengea na kujisimikia nguzo inayokuwa kwenye Bonde la Mufalme, maana alisema: “Mimi sina mutoto mwanaume wa kudumisha jina langu kusudi nikumbukwe.” Nguzo hiyo aliipa jina lake, na inaitwa “Nguzo ya Abusaloma” mpaka leo.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




2 Samweli 18:18
13 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Wakasema: “Tujijengee muji na munara ambao chongo yake itafika mbinguni kusudi tujipatie sifa, kusudi tusisambazwe katika dunia yote.”


Muji ule ukaitwa Babeli, kwa sababu kule ndiko Yawe alikovuruga luga ya dunia yote, na tokea kule akawatawanya watu kila pahali katika dunia.


Abramu aliporudi kisha kumushinda mufalme Kedorilaomeri na wenzake, mufalme wa Sodoma akatoka na kwenda kukutana naye katika bonde la Sawe ni kusema bonde la Mufalme.


Abusaloma alizaa watoto watatu wanaume pamoja na binti mumoja jina lake Tamari. Tamari alikuwa na sura nzuri.


Wazao wake wote wakufe; jina lake lisahauliwe katika kizazi kinachokuja!


Inaonekana wazi kuwa hata wenye hekima wanakufa, nao wapumbafu na wajinga vilevile. Wote wanawaachia wengine mali zao.


Una haki gani kuwa huku? Una ndugu yeyote hapa, hata ukajichongea kaburi ndani ya jiwe juu ya mulima?


Yawe anasema hivi: Muandike mutu huyu kwamba hana watoto, ni mutu ambaye hatafanikiwa katika maisha yake. Maana hakuna hata mumoja wa wazao wake atakayekiikalia kiti cha kifalme cha Daudi na kutawala tena katika Yuda.


Mara moja jambo hilo juu ya mufalme Nebukadneza likatimizwa. Alifukuzwa mbali na wanadamu, akakuwa anakula majani kama ngombe. Alilowanishwa na umande wa mbinguni, na nywele zake zikakuwa ndefu kama manyoya ya tai, na kucha zake kama za ndege.


Naye Noba akashambulia na kuteka Kenati na vijiji vyake, akauita Noba, jina lake mwenyewe.


Samweli alisikia kwamba Saulo alikuwa amekwenda kule Karmeli na amesimamisha munara wa ukumbusho wake, na kwamba amekwenda Gilgali. Hivyo, kesho yake, Samweli aliamuka asubui mapema, akaenda kukutana na Saulo.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ