Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




2 Samweli 18:17 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

17 Wakamukamata Abusaloma, wakamutupia ndani ya shimo kubwa katika pori na kulundika lundo kubwa sana la mawe juu yake. Watu wote wa Israeli wakakimbia, kila mumoja kwake.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




2 Samweli 18:17
15 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Mufalme alijifunika uso wake na kulia kwa sauti kubwa akisema: “Ole mwana wangu Abusaloma! Ole, Abusaloma, mwana wangu! Mwana wangu!”


Sasa, simama uzungumuze na watumishi wako kwa upole. Maana, ninaapa kwa Yawe, kama hauendi kuzungumuza nao, hakuna hata mumoja atakayebaki pamoja nawe leo magaribi. Hili litakuwa jambo baya zaidi kwako kuliko maovu yote yaliyokupata tangu ujana wako mpaka leo.”


Kisha, mufalme akatoka, akaenda, akaikaa kwenye nafasi yake karibu na mulango. Watu wote walipoambiwa kwamba mufalme yuko kwenye mulango, wote walimwendea. Wakati ule, watu wote wa Israeli walikuwa wamekimbia, kila mumoja kwake.


Sasa ilitokea kwamba kule Gilgali kulikuwa mutu mumoja wa ovyoovyo anayeitwa Seba mwana wa Bikiri, wa kabila la Benjamina. Basi Seba alipiga baragumu, na kusema: “Hatuna ushirika wowote na Daudi; hatuna sehemu yetu katika huyo mwana wa Yese. Enyi watu wa Israeli, kila mumoja ajiendee katika hema yake!”


Kisha, huyo mwanamuke akaenda kwa watu wote katika muji kwa hekima yake. Wakamukata Seba mwana wa Bikiri kichwa, wakakitupa inje kwa Yoabu. Kwa hiyo, Yoabu akapiga baragumu na kuwatawanya watu wake kutoka muji ule wa Abeli. Kila mutu akaenda kwake. Yoabu akarudi kwa mufalme Daudi, kule Yerusalema.


Watu wa Yuda walishindwa na watu wa Israeli na kila mumoja alirudi kwake.


Kwa hiyo Yoramu aliondoka na magari yake yote kwenda Sairi. Wakati wa usiku alitoka na waongozi wake wa magari akawashambulia Waedomu waliokuwa wamemuzunguka. Lakini waaskari wake walikimbilia kwao.


Mwenye haki anakumbukwa kwa baraka, lakini waovu watasahauliwa kabisa.


Wazazi hao watawaambia wazee wa muji: ‘Mutoto wetu ni mwenye kiburi na mwasi, hataki kutusikiliza, ni mulafi na mulevi’.


Hapo watu wa muji huo watamupiga mutoto huyo mawe mpaka akufe. Ndivyo mutakavyokomesha ubaya huo kati yenu. Kila mutu katika Israeli atasikia tukio hilo na kuogopa.


Wakati jua lilipokuwa karibu kutua, Yoshua aliamuru waondolewe juu ya miti walipokuwa wametundikwa na kutupwa katika pango walimokuwa wamejificha. Kisha wakaweka mawe makubwa kwenye mulango wa pango, nayo mawe hayo yako kule mpaka leo.


Halafu wakalundika mawe mengi juu yake, ambayo yako mpaka leo. Hapo hasira ya Yawe ikapoa; na pahali pale pakaitwa Bonde la Akori, ni kusema Bonde la Taabu, mpaka hivi leo.


Kisha akamutundika mufalme wa Ai juu ya muti wa tini mpaka magaribi. Lakini jua lilipoanza kutua, Yoshua aliamuru maiti yake iondolewe juu ya muti na kutupwa kwenye mulango wa muji kisha walundike lundo kubwa la mawe juu ya maiti hiyo. Lundo hilo liko kule mpaka leo.


Wafilistini walipiga vita, na Waisraeli walishindwa na kukimbia kila mutu kwake. Siku hiyo kulikuwa mauaji makubwa maana waaskari wa miguu elfu makumi tatu wa Israeli waliuawa.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ