Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




2 Samweli 18:14 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

14 Yoabu akamwambia: “Mimi sina wakati wa kupoteza pamoja nawe.” Yoabu akatwaa mikuki midogo mitatu katika mukono wake, akaenda na kumuchoma Abusaloma ndani ya moyo, Abusaloma akiwa angali muzima kwenye tawi la muti wa mwalo.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




2 Samweli 18:14
14 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kwa hiyo basi, kwa sababu umenizarau na umemutwaa muke wa Uria wa Hiti kuwa muke wako, mauaji hayataondoka katika jamaa yako.’


Basi, Abusaloma akawaambia watumishi wake: “Muangalie, Yoabu ana shamba la shayiri karibu na langu. Muende mulichome kwa moto.” Kwa hiyo watumishi wa Abusaloma wakalichoma shamba la Yoabu kwa moto.


Kisha, vijana kumi waliomubebea Yoabu silaha, wakakuja kumuzunguka Abusaloma, wakamupiga na kumwua.


Mufalme akawaamuru Yoabu, Abisayi na Itayi: “Kwa ajili yangu, mumutendee yule kijana Abusaloma kwa upole.” Watu wote walimusikia mufalme alipoamuru wakubwa wake juu ya Abusaloma.


Hapo mufalme alishikwa na huzuni kubwa, akapanda kwenye chumba kilichokuwa juu ya mulango na kulia. Alipokuwa anapanda, alilia akisema: “Mwana wangu Abusaloma, mwana wangu Abusaloma! Ingekuwa heri ningalikufa pahali pako! Ole, Abusaloma mwana wangu! Mwana wangu!”


Tena Abusaloma ambaye tulimupakaa mafuta akuwe mufalme wetu, sasa ameuawa katika vita. Sasa, kwa nini hatuzungumuzii juu ya kumurudisha mufalme Daudi?”


mwovu atajiona ameshinda kwa muda tu, furaha ya asiyemwogopa Mungu ni ya muda mufupi tu!


Nilimwona mwovu aliyejivuna sana, akinyanyua shingo juu kama mierezi ya Lebanoni!


Songa mbele kwa utukufu upate ushindi, utetee ukweli na kulinda haki. Mukono wako utende mambo makubwa.


Kwa maana, kama vile Yona alivyobaki ndani ya tumbo la samaki mukubwa kwa muda wa siku tatu, muchana na usiku, ndivyo vilevile Mwana wa Mutu atakavyobaki ndani ya udongo kwa muda wa siku tatu, muchana na usiku.


Watu watakapokuwa wakisema: “Kuna amani na usalama”, ndio wakati uharibifu utakapowapata kwa rafla kama vile maumivu ya kuzaa yanavyomupata mwanamuke mwenye mimba, wala hawataweza kuponyoka.


Lakini Yaeli, muke wa Heberi, akatwaa musumari wa kufungia hema na nyundo, akamwendea polepole akaupigilia ule musumari wa kufungia hema katika paji la uso wake ukapenya mpaka katika udongo, kwa maana alikuwa amelala usingizi muzito sababu ya muchoko. Basi, Sisera akakufa palepale.


Kwa mukono mumoja akashika musumari wa kufungia hema, na kwa mukono wake wa kuume nyundo ya fundi. Alimuponda Sisera kichwa, akavunja na kupasuapasua paji lake.


“Ee Yawe, waangamie waadui zako wote! Lakini warafiki zako wakuwe kama jua, wakati linapochomoza kwa mwangaza mukubwa!” Inchi ya Waisraeli ikakuwa na amani kwa muda wa miaka makumi ine.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ