Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




2 Samweli 17:27 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

27-29 Daudi alipofika Mahanaimu, alikutwa na Sobi mwana wa Nahasi wa muji wa Raba katika inchi ya Amoni, Makiri mwana wa Amieli wa muji wa Lodebari, pamoja na Barzilayi wa muji wa Rogelimu katika inchi ya Gileadi. Hawa watu waliona kwamba Daudi na watu wake walikuwa na njaa, walikuwa wanachoka na walikuwa na kiu kwa sababu ya kusafiri katika jangwa. Basi, waliwapelekea vitanda, mabeseni, vyombo vya udongo, ngano, shayiri, unga, mihindi yenye kukaangwa, kunde na manjegere, asali, siagi, kondoo na maziwa kutoka nyama wao wa kufugwa.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




2 Samweli 17:27
9 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Wakati ule, Yoabu aliushambulia Raba muji wa Waamoni, naye akauteka muji ule wa kifalme.


Abusaloma pamoja na watu wa Israeli walipiga kambi yao katika inchi ya Gileadi.


Mufalme akamwuliza: “Yuko wapi?” Siba akamujibu: “Yuko kwenye nyumba ya Makiri mwana wa Amieli kule Lodebari.”


“Lakini uwatendee mema wana wa Barzilayi, yule Mugileadi, wakuwe kati ya wale wanaokula kwenye meza yako, kwa sababu walinitendea mema wakati nilipomukimbia ndugu yako Abusaloma.


Watu wa ukoo hizi za makuhani vilevile walirudi: ukoo wa Habaya, wa Hakosi na wa Barzilayi. Huyo Barzilayi alikuwa ameoa binti ya Barzilayi wa Gileadi, naye vilevile akaitwa Barzilayi.


Mufalme Nahasi wa Waamoni, alikwenda na kuushambulia muji wa Yabesi-Gileadi. Wakaaji wa muji wa Yabesi-Gileadi wakamwambia Nahasi: “Fanya mapatano nasi, nasi tutakutumikia.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ