Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




2 Samweli 17:25 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

25 Wakati ule, Abusaloma alikuwa amemuweka Amasa kuwa jemadari wa waaskari pahali pa Yoabu. Amasa alikuwa mwana wa Itira, Mwisimaeli. Mama yake aliitwa Abigaili binti wa Nahasi, aliyekuwa dada ya Zeruya mama ya Yoabu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




2 Samweli 17:25
11 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Abusaloma pamoja na watu wa Israeli walipiga kambi yao katika inchi ya Gileadi.


Ninyi ni wandugu zangu, ninyi ni damu yangu. Kwa nini mukuwe wa mwisho kunirudisha mimi mufalme kwangu?


Muulize vilevile Amasa kama yeye si damu yangu. Tena Mungu aniue ikiwa simufanyi yeye kuwa jemadari wa kundi langu la waaskari tangu leo pahali pa Yoabu.’ ”


Kisha, mufalme akamwambia Amasa: “Unikusanyie watu wote wa Yuda katika siku tatu, na wewe mwenyewe ukuwe pale.”


Yoabu alipopata habari, alikimbilia katika hema ya Mungu na kushikilia pembe za mazabahu kwa maana alikuwa amemwunga Adonia mukono ingawa mbele hakukuwa na Abusaloma.


Mungu atamwazibu Yoabu kwa mauaji hayo aliyoyafanya bila baba yangu kuwa na habari. Yeye aliwaua watu wawili ambao walikuwa wa maana zaidi kuliko yeye, tena walimupita kwa wema; aliwaua Abeneri mwana wa Neri, jemadari wa kundi la waaskari Waisraeli, na Amasa mwana wa Yeteri, jemadari wa waaskari wa Yuda.


“Zaidi ya hayo, unajua vilevile yale Yoabu mwana wa Zeruya aliyonitendea, jinsi alivyowatendea majemadari wawili wa waaskari wa Israeli, Abeneri mwana wa Neri, na Amasa mwana wa Yeteri. Aliwaua wakati wa amani akitaka kulipiza kisasi kwa mauaji waliyofanya wakati wa vita. Aliwaua watu wasiokuwa na kosa, nami nikabeba lazima ya kifo cha watu wale kwa ajili ya vitendo vyake.


Halafu Roho akamujaza Amasai, mukubwa wa wale watu makumi tatu, naye akasema: “Sisi ni watu wako, ee Daudi! Tuko upande wako, ee mwana wa Yese! Amani, amani ikuwe kwako, na amani ikuwe kwa yeyote anayekusaidia! Maana Mungu wako ndiye anayekusaidia.” Kisha Daudi akawapokea na kuwafanya wakubwa katika kundi lake.


Yese alizaa: Eliabu, muzaliwa wake wa kwanza, wa pili Abinadabu, wa tatu Simea,


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ