Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




2 Samweli 17:17 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

17 Wakati ule, Yonatani na Ahimasi walikuwa wakimungojea karibu na Eni-Rogeli, kusudi wasionekane na mutu yeyote wakiingia katika muji. Kila mara mujakazi fulani alikuwa akiwapelekea habari nao wakaipeleka kwa mufalme Daudi.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




2 Samweli 17:17
8 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Mufalme Daudi akamwambia tena Zadoki: “Twaa mwana wako Ahimasi na Yonatani mwana wa Abiatari, murudi katika muji kwa amani.


Makuhani Zadoki na Abiatari wako pamoja nawe katika muji. Basi, chochote utakachosikia kutoka katika nyumba ya mufalme, uwaambie makuhani Zadoki na Abiatari.


Watoto wao wawili wanaume, Ahimasi mwana wa Zadoki na Yonatani mwana wa Abiatari, wako pamoja nao. Na neno lolote mutakalosikia mutanipasha habari kwa njia yao.”


Alipokuwa akisema, Yonatani mwana wa kuhani Abiatari akaingia. Adonia akasema: “Karibu, maana wewe ni mutu hodari na unaleta habari nzuri.”


Siku moja, Adonia alitoa sadaka ya kondoo, ngombe na wana-ngombe wanono kwenye Jiwe la Zoheleti, karibu na chemichemi inayoitwa Enrogeli. Akawaalika kwenye karamu ya sadaka hiyo wandugu zake wote, ni kusema wana wengine wa mufalme, na watumishi wote wa mufalme wanaokuwa wa kabila la Yuda.


Kutoka hapo, uliendelea mpaka Debiri kwenye bonde la Akori na kaskazini kuelekea Gilgali, karibu na mwinuko wa Adumimu ambao uko upande wa kusini wa kijito, kisha ukaelekea kwenye chemichemi za Eni-Semesi na kuishia Eni-Rogeli.


Kisha ulielekea chini kupitia pembeni ya mulima unaokuwa karibu na bonde la mwana wa Hinomu, ambalo lilikuwa katika sehemu ya kaskazini zaidi ya bonde la Warefaimu. Halafu mupaka uliteremuka kuelekea bonde la Hinomu, upande wa kusini wa kilima cha Wayebusi, ukaendelea kuteremuka mpaka Eni-Rogeli.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ