Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




2 Samweli 16:21 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

21 Ahitofeli akamwambia Abusaloma: “Ulale na wale wahabara za baba yako ambao aliwaacha kuangalia nyumba yake. Kisha watu wote wa Israeli watakaposikia kwamba umechukizwa na baba yako, hapo watu wote wanaokuwa pamoja nawe watapata nguvu.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




2 Samweli 16:21
22 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Basi, Yakobo akamwambia Simeoni na Lawi: “Ninyi mumeniletea taabu kwa kunifanya nichukiwe na wakaaji wa inchi hii ya Wakanana na Waperizi. Mimi sina watu wengi, na kama wakikusanyika kwa kunishambulia wataniangamiza mimi pamoja na jamaa yangu.”


Wakati Israeli alipokuwa anakaa katika inchi ile, mwana wake Rubeni, akalala na Biliha, habara ya baba yake. Naye Israeli akasikia habari hizo. Yakobo alikuwa na wana kumi na wawili.


Halafu, bila kujua kwamba huyo alikuwa muke wa mwana wake, akamwendea pale kando ya njia, akamwambia: “Ninataka kulala nawe.” Tamari akamwuliza: “Utanipa nini upate kulala nami?”


Katika siku zile na hata kisha, kulikuwa majitu katika dunia ambao walikuwa wazao wa wana wa Mungu na wabinti za wanadamu. Hao ndio watu waliokuwa mashujaa na wenye sifa wa zamani, na waliitwa Wanefili.


Waamoni walipoona kwamba wamemuchukiza Daudi, walijilipia waaskari wa miguu wa Waaramu elfu makumi mbili kutoka Beti-Rehobu na Zoba, waaskari elfu kumi na mbili kutoka Tobu, na mufalme Maka akiwa na waaskari elfu moja.


Sikiliza, Yawe anasema: ‘Nitaleta hasara katika jamaa yako mwenyewe. Nitawatwaa wake zako ukiona kwa macho yako mwenyewe na kumupa jirani yako, naye atalala nao waziwazi.


Yonadabu akamwambia: “Wewe ujilalishe katika kitanda na ujifanye kuwa mugonjwa. Baba yako atakapokuja kukuona, wewe umusihi ukisema: ‘Umuruhusu dada yangu, Tamari, akuje aniletee mukate nipate kula na anitayarishie chakula mbele yangu kusudi nikione naye mwenyewe anikulishe.’ ”


Basi, mufalme akaondoka pamoja na jamaa yake, lakini akawaacha wahabara wake kumi wakishugulika na kazi za nyumba.


Halafu Abusaloma alimwambia Ahitofeli: “Unipatie shauri; tufanye nini?”


Husayi akamwambia Abusaloma: “Wakati huu, shauri Ahitofeli alilolitoa si jema.”


Lakini mukuwe imara na mashujaa. Saulo, bwana wenu, amekufa, na watu wa Yuda wamenipakaa mafuta nikuwe mufalme wao.”


Nyuma, Daudi alifika katika nyumba yake kule Yerusalema. Mufalme aliwatwaa wahabara wake kumi ambao alikuwa amewaacha kwa kuangalia nyumba yake, akawaweka kwenye nyumba moja wapate kulindwa, akawatunza vizuri, lakini hakulala nao. Kwa hiyo wahabara hao wakakuwa wakifungwa mpaka siku za kufa kwao, wakaishi kama vile walikuwa wajane.


Resoni alikuwa adui wa Waisraeli siku zote za utawala wa Solomono, akamusumbua sana Solomono kama naye Hadadi alivyomusumbua. Basi, Resoni aliizarau inchi ya Israeli, naye alitawala inchi ya Aramu.


Naye akasema: “Tafazali, ninakusihi umwombe mufalme Solomono aniruhusu nimukamate Abisagi, yule Musunami, akuwe muke wangu, kwa maana ninajua hatakukatalia wewe.”


Mufalme Solomono akamwuliza mama yake: “Kwa nini unataka nimupe Abisagi? Hii ni sawa kabisa na kumutakia ufalme wangu! Kumbuka kwamba yeye ni mukubwa yangu, na si ile tu, kuhani Abiatari na jemadari Yoabu mwana wa Zeruya, wako upande wake!”


Usimuvunjie heshima baba yako kwa kulala na mumoja wa wake zake. Hao ni wamama zako.


Mwanaume akilala na mumoja wa wake za baba yake, anamupatisha baba yake haya, wote wawili wanapaswa kuuawa. Mwanaume huyo na mwanamuke huyo wote wawili watauawa na damu yao itakuwa juu yao wenyewe.


Enyi watu wa Yuda na watu wa Israeli! Wakati uliopita ninyi mulionekana kuwa watu waliolaaniwa kati ya watu wa mataifa. Lakini sasa mimi nitawaokoa, nanyi mutakuwa watu waliobarikiwa. Basi, musiogope tena, lakini mujipe moyo!


Habari inasikilika fasi zote kwamba kunafanyika uzinzi katikati yenu. Wanaeleza kwamba uzinzi huu ni ubaya mukubwa, usiofanyika hata katikati ya wapagani, kwa maana wanasema kwamba kuna mumoja wenu ambaye amekamata muke wa baba yake kuwa muke wake!


Waisraeli wote walisikia kwamba Saulo alikuwa ameishinda kambi ya waaskari walinzi wa Wafilistini, na kwamba Wafilistini wanawachukia sana Waisraeli. Waliitwa kwenda kuungana na Saulo kule Gilgali.


Kwa hiyo, Akisi alimusadiki Daudi, akifikiri: “Wanainchi wenzake Waisraeli hawamupendi kabisa. Kwa hiyo, atanitumikia maisha yake yote.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ