Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




2 Samweli 16:11 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

11 Tena mufalme Daudi akamwambia Abisayi na hata watumishi wake wote: “Ikiwa mutoto wangu mwenyewe anayawinda maisha yangu, si ni zaidi kwa mutu wa kabila la Benjamina? Ninyi muache anilaani maana Yawe amemwagiza anilaani.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




2 Samweli 16:11
14 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Halafu neno la Yawe lilimufikia kusema hivi: “Huyu hatakuwa murizi wako! Mwana wako atakayetoka katika tumbo lako ndiye atakayekuwa murizi wako.”


Lakini sasa musifazaike wala kuhuzunika kwa kuniuzisha. Mungu ndiye aliyenileta huku niwatangulie, kusudi niyaokoe maisha ya watu.


Sasa ilitokea kwamba kule Gilgali kulikuwa mutu mumoja wa ovyoovyo anayeitwa Seba mwana wa Bikiri, wa kabila la Benjamina. Basi Seba alipiga baragumu, na kusema: “Hatuna ushirika wowote na Daudi; hatuna sehemu yetu katika huyo mwana wa Yese. Enyi watu wa Israeli, kila mumoja ajiendee katika hema yake!”


mufalme Daudi akamwambia nabii Natani: “Angalia, mimi ninakaa katika nyumba iliyojengwa na miti ya mierezi, lakini Sanduku la Mungu linakaa ndani ya hema.”


Siku moja wakati Saniharibu alipokuwa akiabudu katika nyumba ya Nisiroki mungu wake, wana wake wawili, Adarameleki na Sarezeri walimwua kwa upanga, halafu wakakimbilia katika inchi ya Ararati. Halafu mwana wake Esari-Hadoni akatawala kwa pahali pake.


Naye Yawe akatuma malaika aliyewaua waaskari shujaa, majemadari na wakubwa katika kambi ya mufalme wa Asuria. Basi, mufalme wa Asuria akarudia katika inchi yake akijaa haya. Mara tu alipoingia ndani ya nyumba ya mungu wake, wana wake mwenyewe wakamwua palepale kwa upanga.


Uwaache walaani, lakini wewe unibariki; wanaonishambulia wafezeheke, nami mutumishi wako nifurahi.


Na ikiwa nabii yule akidanganyika na kusema kitu, basi mimi Yawe nimemupotosha. Nami nitanyoosha mukono wangu kwa kumwondoa nabii yule kutoka kwa watu wangu Waisraeli.


Tena niliwapa masharti mabaya na maagizo ambayo hayawezi kuwawezesha kuishi.


“Ndugu atamutoa ndugu, kusudi auawe, na baba atamutoa mutoto wake, nao watoto watawageukia wazazi wao na kuwaua.


Basi, sasa bwana wangu mufalme, usikie maneno ya mutumishi wako. Ikiwa Yawe ndiye aliyekuchochea ukuje kunishambulia, basi, apokee sadaka ambayo itamusukuma kubadilisha mawazo yake. Lakini ikiwa ni watu, basi, Yawe awalaani watu hao maana wamenifukuza kutoka urizi ambao Yawe aliotupa wakisema: ‘Kwenda uitumikie miungu mingine.’


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ