Urudi Yerusalema na kumwambia Abusaloma: ‘Nitakuwa mutumishi wako, ee mufalme, kama vile nilivyokuwa zamani mutumishi wa baba yako’. Kwa njia hiyo utanisaidia kupinga mashauri ya Ahitofeli.
Watoto wao wawili wanaume, Ahimasi mwana wa Zadoki na Yonatani mwana wa Abiatari, wako pamoja nao. Na neno lolote mutakalosikia mutanipasha habari kwa njia yao.”
Wakati ule, Yonatani na Ahimasi walikuwa wakimungojea karibu na Eni-Rogeli, kusudi wasionekane na mutu yeyote wakiingia katika muji. Kila mara mujakazi fulani alikuwa akiwapelekea habari nao wakaipeleka kwa mufalme Daudi.
Kisha, Ahimasi mwana wa Zadoki, akasema: “Uniruhusu nikimbie kumupelekea mufalme habari hizi kwamba Yawe amemukomboa toka katika nguvu za waadui zake.”
Yule mutumishi akamwambia: “Ngoja kidogo. Katika muji huu kuna mutu wa Mungu ambaye anaheshimiwa sana. Kila neno analosema linakuwa kweli. Sasa tumwendee. Labda anaweza kutuambia jinsi safari yetu itakavyokuwa.”
(Hapo zamani katika Israeli kama mutu akitaka kumwomba Mungu shauri, alisema: “Basi, kuja, kuja tuende kwa mwonaji.” Maana mutu anayeitwa nabii siku hizi hapo zamani aliitwa mwonaji).