Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




2 Samweli 15:24 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

24 Kuhani Abiatari akatoka, hata na kuhani Zadoki akatoka pamoja na Walawi wote wakilibeba Sanduku la Agano la Mungu. Wakaliweka lile Sanduku la Mungu chini, mpaka watu wote walipopita kutoka Yerusalema.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




2 Samweli 15:24
23 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Mufalme Daudi akamwambia tena Zadoki: “Twaa mwana wako Ahimasi na Yonatani mwana wa Abiatari, murudi katika muji kwa amani.


Makuhani Zadoki na Abiatari wako pamoja nawe katika muji. Basi, chochote utakachosikia kutoka katika nyumba ya mufalme, uwaambie makuhani Zadoki na Abiatari.


Sewa alikuwa katibu. Zadoki na Abiatari walikuwa makuhani.


Watu wale waliolibeba Sanduku la Yawe kila mara walipopiga hatua sita, Daudi alitoa sadaka: ngombe dume na mwana-ngombe mumoja wenye kunona.


Zadoki mwana wa Ahitubu na Ahimeleki mwana wa Abiatari walikuwa makuhani. Seraya alikuwa katibu.


Lakini kuhani Zadoki, Benaya mwana wa Yehoyada, nabii Natani na Simei, na Rei pamoja na walinzi wa Daudi, hawakumwunga Adonia mukono.


Mufalme Solomono akamwambia kuhani Abiatari: “Ondoka uende katika shamba lako, kule Anatoti. Unastahili kufa wewe. Lakini sasa, sitakuua kwa sababu ulilishugulikia Sanduku la Agano la Yawe ulipokuwa na baba yangu Daudi, ukateswa pamoja naye.”


Mufalme akamuweka Benaya mwana wa Yehoyada kuwa jemadari wa kundi la waaskari kwa pahali pa Yoabu, na Zadoki akakuwa kuhani pahali pa Abiatari.


Kisha akasema: “Hakuna mutu mwingine yeyote atakayebeba Sanduku la Agano isipokuwa Walawi, maana Yawe aliwachagua wao kwa kulibeba na kumutumikia kwa milele.”


Eneo hilo litakuwa kwa ajili ya makuhani wa uzao wa Zadoki, ambao walinitumikia kwa uaminifu na hawakuasi wakati Waisraeli walipoasi kama Walawi walivyofanya.


Kisha Haruni na wana wake kufunika Pahali Patakatifu pamoja na vyombo na vifaa vyake vyote, wakiwa tayari kuanza safari, watu wa ukoo wa Kohati watakuja na kuvibeba. Lakini wao, hawaruhusiwi kabisa kugusa vyombo hivyo vitakatifu, kusudi wasikufe. Hiyo ndiyo kazi ya ukoo wa Kohati kila wakati hema la mukutano linapohamishwa.


Lakini Musa hakuwapa Wakohati kitu chochote kwa sababu wao walikuwa na utumishi wa kutunza vitu vitakatifu ambavyo vilipaswa kubebwa juu ya mabega.


wakawaambia watu: “Mutakapoliona Sanduku la Agano la Yawe, Mungu wenu, limebebwa na makuhani Walawi, mutaondoka na kulifuata;


Kisha akawaambia makuhani: “Mutwae Sanduku la Agano, mutangulie nalo mbele ya watu.” Nao wakalitwaa na kutangulia mbele ya watu.


Makuhani saba, kila mumoja akiwa anabeba baragumu yake ya pembe ya kondoo dume, watatangulia mbele ya Sanduku la Agano. Katika siku ya saba mutauzunguka muji ule mara saba, nao makuhani wakipiga mabaragumu.


Basi, Yoshua mwana wa Nuni, akawaita makuhani, akawaambia: “Mulibebe Sanduku la Agano na makuhani saba watwae mabaragumu saba ya kondoo dume, watangulie mbele ya Sanduku la Yawe.”


Lakini Abiatari, mumoja wa watoto wa kiume wa Ahimeleki mwana wa Ahitubu, aliponyoka akakimbilia kwa Daudi.


Sanduku la Agano la Mungu lilitekwa, na wale wana wawili wa Eli, Hofuni na Finehasi, wakauawa.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ