Lakini Itayi akamujibu mufalme: “Kama vile Yawe anavyoishi na kama vile bwana wangu mufalme anavyoishi, popote utakapokuwa, ikiwa ni kwa kufa au ni kwa kuishi, nami mutumishi wako nitakuwa pale.”
Daudi alipokuwa akipita pamoja na watu wake, watu wote katika inchi yote walilia kwa sauti. Mufalme Daudi akavuka kijito cha Kidroni pamoja na watu wote, wakapita kuelekea katika jangwa.