15 Watumishi wake wakamwambia: “Sisi watumishi wako, bwana wetu mufalme, tuko tayari kufanya neno lolote unaloamua.”
Basi, Daudi akawaambia watumishi wake waliokuwa naye Yerusalema: “Musimame tukimbie, kama sivyo, hatutaweza kumuponyoka Abusaloma. Tufanye haraka kuondoka kusudi asituletee hasara na kuuangamiza muji kwa upanga.”
Basi, mufalme akaondoka pamoja na jamaa yake, lakini akawaacha wahabara wake kumi wakishugulika na kazi za nyumba.
Kisha, Siba akamwambia mufalme: “Mimi mutumishi wako, nitafanya yote kulingana na amri yako.” Basi, Mefiboseti akakuwa anapata chakula chake kwenye meza ya Daudi, kama vile mumoja wa watoto wa mufalme.
Warafiki wengi wanaweza kumwangusha mutu, lakini kuna rafiki mwaminifu kuliko ndugu.
Ninyi ni warafiki zangu, kama mukifanya sawa ninavyowaagiza.
Yule kijana aliyemubebea silaha akamwambia: “Fanya chochote unachotaka kufanya, mimi niko pamoja nawe maana wazo lako ndilo wazo langu.”