Siku iliyofuata, mutu mumoja kutoka kambi ya Saulo, nguo zake zikiwa zimepasuka kwa huzuni na akiwa na mavumbi juu ya kichwa, alimwendea Daudi. Alipomufikia Daudi, alijitupa uso mpaka chini mbele yake kwa heshima.
Halafu Ahimasi akamwambia mufalme kwa sauti kubwa: “Mambo yote ni sawa.” Akainama mbele ya mufalme, kwa heshima na kusema: “Yawe atukuzwe, Mungu wako, ambaye amekukomboa kutoka watu walioinua mikono yao juu yako, bwana wangu mufalme.”
Yule kijana alipokwisha kuondoka, Daudi akasimama na kutoka pahali alipojificha karibu na lundo la mawe. Aliinama chini kwa heshima mara tatu mbele ya Yonatani. Wote wawili, Daudi na Yonatani, wakakumbatiana na kulia. Daudi alikuwa na uchungu zaidi kuliko Yonatani.