Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




2 Samweli 14:32 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

32 Abusaloma akamujibu: “Nilikutumia ujumbe, ukuje huku kusudi nikutume kwa mufalme, umwulize: ‘Kwa nini niliondoka Gesuri? Ingekuwa bora kwangu kubaki kule.’ Sasa unisaidie nipate kumwona mufalme. Kama nina kosa basi, aniue!”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




2 Samweli 14:32
15 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Yule mwanaume akajibu: “Mwanamuke uliyenipa akae pamoja nami ndiye aliyenipa tunda la muti ule, nami nikakula.”


Lakini Abusaloma alikimbilia kwa Talmayi mwana wa Amihudi, mufalme wa muji wa Gesuri. Mufalme Daudi akamufanyia mwana wake Amunoni kilio kwa siku nyingi.


Yoabu akaenda kwa Abusaloma akamwuliza: “Kwa nini watumishi wako wamechoma shamba langu?”


Kiliabu muzaliwa wake wa pili, mama yake alikuwa Abigaili mujane wa Nabali wa muji wa Karmeli; Abusaloma muzaliwa wake wa tatu, mama yake alikuwa Maka binti ya Talmayi mufalme wa Gesuri;


Zambi inaongea na mutu mwovu, ndani kabisa ya moyo wake; kuogopa Mungu si kitu kwake.


Hatukukuambia mambo haya tulipokuwa bado Misri? Tulikuambia utuache tuendelee kuwatumikia Wamisri. Ingalikuwa vizuri kuwatumikia Wamisri kuliko kukufia huku katika jangwa.”


“Heri Yawe angelituua tulipokuwa katika inchi ya Misri ambako tulikaa, tukakula nyama na mikate hata tukashiba. Lakini ninyi mumetuleta huku katika jangwa kwa kuua jamii hii yote kwa njaa!”


Lakini wote walikuwa na kiu, wakamunungunikia Musa wakisema: “Kwa nini ulitutoa kule Misri utuue kwa kiu, sisi wote na watoto wetu na mifugo yetu?”


Anayeficha makosa yake hatafanikiwa, lakini anayeungama na kuyaacha atahurumiwa.


Walisikia haya walipotenda machukizo hayo? Hapana, hawakusikia haya hata kidogo. Hata zamiri hazikuwagonga. Kwa hiyo, wataanguka pamoja na wale walioanguka; nitakapowaazibu, wataangamia. –Ni Yawe anayesema hivyo.


Halafu nao watajibu: ‘Bwana, ni wakati gani tulipokuona ukisikia njaa, au kiu, au ukikuwa mugeni, au uchi, au mugonjwa, au mufungwa, nasi hatukukusaidia?’


Basi tunajua kama maneno yote yanayosemwa na Sheria, yanawaelekea wale wanaolazimishwa kutii Sheria, kusudi mutu yeyote asikuwe na namna ya kujitetea, na dunia nzima ipaswe kuhukumiwa na Mungu.


Samweli alipomufikia Saulo, Saulo akamwambia Samweli: “Yawe akubariki! Nimetimiza amri ya Yawe.”


Hivyo unitendee mema maana umefanya agano nami, mimi mutumishi wako, mbele ya Yawe. Lakini, kama nimefanya kosa basi, uniue wewe mwenyewe. Kwa nini unipeleke kwa baba yako kusudi aniue?”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ