Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




2 Samweli 14:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Halafu uende kwa mufalme umwambie yale ninayokuambia.” Kisha Yoabu akamwambia maneno ya kumwambia mufalme.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




2 Samweli 14:3
9 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Mufalme akamwuliza: “Haukupatana na Yoabu katika jambo hili?” Yule mwanamuke akasema: “Kama vile unavyoishi mwenyewe bwana wangu mufalme, mutu hawezi kupita pembeni juu ya jambo ulilosema bwana wangu mufalme. Yoabu yule mutumishi wako ndiye aliyenituma. Ni yeye aliyeniambia maneno yote haya niliyokuambia mimi mujakazi wako.


Huyo mwanamuke kutoka Tekoa akaenda kwa mufalme, akainama uso mpaka chini mbele ya mufalme, akamwambia: “Ee mufalme, unisaidie.”


Nikawatuma kwa Ido, kiongozi wa jamii ya watu kule Kasifia, nikimwomba yeye pamoja na wenzake watumishi wa nyumba ya Mungu, watuletee watu watakaotumika katika nyumba ya Mungu.


Wewe utaongea naye na kumwambia yote atakayosema. Mimi nitawasaidia na kuwafundisha mambo mutakayofanya.


Nimeyaweka maneno yangu katika kinywa chako; nimekuficha katika kivuli cha mukono wangu. Mimi nilizitandaza mbingu, nikaiweka misingi ya dunia. Mimi ninawaambia, enyi watu wa Sayuni: Ninyi ni watu wangu.


Yawe anasema: Mimi ninafanya nanyi agano hili: Roho wangu anayekuwa juu yenu, maneno niliyoyaweka katika kinywa chenu, hayataondoka kwenu hata kidogo, wala kwa watoto na wajukuu wenu, tangu sasa na hata milele.


Kisha Yawe akanyoosha mukono wake, akagusa kinywa changu, akaniambia: Nimetia maneno yangu ndani ya kinywa chako.


Yawe akamupa Balamu maneno atakayosema na kumwambia arudi kwa Balaki.


Nitawachagulia kati ya wandugu zao wenyewe nabii kama wewe, nitatia maneno yangu ndani ya kinywa chake, naye atawaambia yote nitakayomwamuru.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ