Siku moja, wakati wa magaribi, Daudi aliamuka toka katika kitanda, akaenda kwenye dari ya nyumba ya kifalme. Alipokuwa anatembea kule juu, alimwona mwanamuke mumoja akioga na mwanamuke yule alikuwa muzuri sana kwa umbo.
Abusaloma, alipokuwa angali anaishi, alikuwa amejijengea na kujisimikia nguzo inayokuwa kwenye Bonde la Mufalme, maana alisema: “Mimi sina mutoto mwanaume wa kudumisha jina langu kusudi nikumbukwe.” Nguzo hiyo aliipa jina lake, na inaitwa “Nguzo ya Abusaloma” mpaka leo.
Nitaushambulia muji wa Babeli na kuuangamiza kabisa. –Ni ujumbe wa Yawe wa majeshi.– Nitaharibu kila kitu, muji wote, watoto na yeyote aliyebaki muzima. –Ni ujumbe wa Yawe.–
Yawe anasema hivi: Muandike mutu huyu kwamba hana watoto, ni mutu ambaye hatafanikiwa katika maisha yake. Maana hakuna hata mumoja wa wazao wake atakayekiikalia kiti cha kifalme cha Daudi na kutawala tena katika Yuda.