Kiliabu muzaliwa wake wa pili, mama yake alikuwa Abigaili mujane wa Nabali wa muji wa Karmeli; Abusaloma muzaliwa wake wa tatu, mama yake alikuwa Maka binti ya Talmayi mufalme wa Gesuri;
Yairi, mutu wa kabila la Manase, alitwaa eneo lote la inchi ya Argobu, ni kusema Basani, mpaka kwenye mupaka wa Gesuri na Maka. Vijiji vyote alivipa jina lake, na mpaka leo vinajulikana kama vile ‘Vijiji vya Yairi’.