2 Samweli 14:20 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
20 Yoabu alifanya hivyo kwa kubadilisha mambo. Lakini, wewe bwana wangu, una hekima kama ya malaika wa Mungu hata unaweza kujua mambo yote yanayokuwa katika dunia.”
Nami mujakazi wako nilifikiri hivi: ‘Neno la bwana wangu mufalme litanipa amani ndani ya moyo, maana wewe bwana wangu mufalme ni kama malaika wa Mungu katika kupambanua mazuri na mabaya.’ Yawe, Mungu wako, akuwe pamoja nawe.”
Mefiboseti akasema: “Ee bwana wangu mufalme, mutumishi wangu alinidanganya. Maana, mimi mutumishi wako, nilimwambia: ‘Unitandikie punda nipate kupanda juu yake kwenda pamoja na mufalme’, maana mimi mutumishi wako ni kilema.
Daudi alipomwomba Yawe shauri, Yawe alimwambia: “Usiwashambulie kutoka hapa unapokuwa, lakini zunguka nyuma yao na kuwashambulia kutokea mbele ya miti ya miforosadi.
Akisi akamwambia: “Ninajua kwamba hauna lawama mbele yangu kama malaika wa Mungu. Hata hivyo, wakubwa wa Wafilistini wamesema: ‘Asiende hata kidogo pamoja nasi katika vita’.