Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




2 Samweli 14:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Kwa hiyo alituma watu kule Tekoa kusudi wamutafutie mwanamuke mwenye hekima. Walipomuleta, akamwambia: “Ujifanye sawa vile mwenye kuwa na kilio. Vaa nguo za kilio, usijipakae mafuta, lakini ujifanye kama mwanamuke ambaye amekuwa katika kilio kwa muda murefu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




2 Samweli 14:2
17 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Basi, Tamari akarudi kwa nyumba akavua kile kitambaa alichojifunika, akavaa tena nguo zake za ujane.


Batiseba muke wa Uria aliposikia kwamba mume wake Uria amekufa, akafanya kilio kwa ajili yake.


Kisha, Daudi akasimama, akaoga, akajipakaa mafuta na kubadilisha nguo zake. Halafu akaenda katika nyumba ya Yawe na kuabudu. Kisha akarudi kwake, akaamuru wamuletee chakula, naye akakula.


Kisha, mwanamuke mumoja mwenye hekima alisikilika kutoka muji akisema: “Musikie! Musikie! Mumwambie Yoabu akuje nizungumuze naye.”


Helesi wa muji Palti; Ira mwana wa Ikesi wa muji Tekoa;


Yeroboamu akamwambia muke wake: “Ujigeuze kusudi watu wasitambue kwamba wewe ni muke wangu, uende Shilo kwa nabii Ahiya aliyesema kwamba mimi nitakuwa mufalme wa Israeli.


Yawe alikuwa amekwisha kumwambia Ahiya kwamba muke wa Yeroboamu alikuwa katika njia, anakuja kumwuliza yatakayomupata mwana wake mugonjwa, na jinsi atakavyomujibu. Muke wa Yeroboamu alipofika, alijisingizia kuwa mutu mwingine.


Kesho yake, wakaamuka asubui mapema, wakaenda mpaka katika jangwa la Tekoa. Walipokuwa wanaondoka, Yosafati akasimama, akawaambia: “Musikilize, enyi watu wa Yuda na wakaaji wa Yerusalema! Mumwamini Yawe, Mungu wenu, nanyi mutakuwa imara. Muwaaminie manabii wake, nanyi mutashinda.”


Sehemu ingine inayofuata, ikitokea kwenye munara murefu mpaka kwenye ukuta wa Ofeli ikajengwa upya na wakaaji wa muji wa Tekoa.


Sehemu inayofuata ikajengwa na watu kutoka muji wa Tekoa. Lakini viongozi wa muji wakakataa kufanya kazi ya mikono waliyoagizwa kufanya na wasimamizi.


apate divai ya kumuchangamusha, mafuta ya muzeituni ya kumwangarisha, na mukate wa kumupa nguvu.


Vaa vizuri, ujipakae mafuta kwenye kichwa.


Enyi watu wa kabila la Benjamina, muondoke Yerusalema, mukimbie! Mupige baragumu katika muji Tekoa! Muonyeshe kitambulisho cha vita huko Beti-Keremu, maana hasara na maangamizi makubwa vinakuja kutoka upande wa kaskazini.


Haya ni maneno ya Amosi, mumoja wa wachungaji wa nyama wa muji wa Tekoa. Mungu alimufunulia Amosi mambo haya yote juu ya inchi ya Israeli miaka miwili mbele ya tetemeko la inchi, wakati Uzia alipokuwa mufalme wa Yuda, na Yeroboamu mwana wa Yoasi alipokuwa mufalme wa Israeli.


Lakini wewe unapofunga kula chakula, unawe uso wako na kuchanua nywele zako,


Kwa hiyo, nawa, ujipake mafuta na kuvaa vizuri, kisha uende kule katika kiwanja pahali anapopepetea. Lakini angalia usijionyeshe kwake mpaka atakapomaliza kula na kunywa.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ