Lakini Abusaloma alikuwa amekwisha kukimbia. Naye kijana aliyekuwa na zamu ya ulinzi, akaona kundi kubwa la watu wanakuja kutokea kwenye mulima katika barabara ya kutoka Horonaimu.
Yule mwanamuke akamwambia: “Kwa nini basi, umepanga kutenda uovu huu juu ya watu wa Mungu? Kulingana na uamuzi wako juu ya jambo hilo, wewe mwenyewe umejihukumu kuwa na kosa kwa sababu haumuruhusu mwana wako arudi kwa nyumba kutoka kule alikokimbilia.
Kiliabu muzaliwa wake wa pili, mama yake alikuwa Abigaili mujane wa Nabali wa muji wa Karmeli; Abusaloma muzaliwa wake wa tatu, mama yake alikuwa Maka binti ya Talmayi mufalme wa Gesuri;