30 Walipokuwa wangali katika njia, Daudi alipata habari kwamba Abusaloma amewaua watoto wake wote hakuna hata mumoja aliyebakia.
Halafu, watumishi wa Abusaloma walimutendea Amunoni kama vile walivyoamriwa na Abusaloma, kisha wana wengine wa mufalme wakaondoka, kila mumoja akapanda juu ya nyumbu wake na kukimbia.
Mufalme Daudi alisimama, akapasua nguo yake kwa huzuni akalala chini. Hata na watumishi wake wote waliokuwa wakisimama karibu naye walipasua nguo zao.
Yefuta alipomwona, akapasua nguo yake kwa huzuni na kusema: “Ee binti yangu! Umenivunja moyo. Wewe umekuwa chanzo kikubwa cha matatizo kwangu. Nimekwisha kumwapia Yawe nami siwezi kuvunja kiapo changu.”