Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




2 Samweli 13:28 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

28 Abusaloma akawaambia watumishi wake: “Mumwangalie Amunoni atakapokuwa amekunywa divai na kufurahi. Nitakapowaambia: ‘Mumupige Amunoni’, mumwue. Hiyo ni amri yangu kwenu. Mujipe moyo na mukuwe hodari.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




2 Samweli 13:28
30 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Akakunywa divai, akalewa, kisha akalala uchi ndani ya hema yake.


Daudi alimwalika Uria kula na kunywa kule kwake, akamulewesha Uria. Hata hivyo, usiku ule Uria hakwenda kwake, lakini alilala kwenye kilalio chake pamoja na watumishi wa bwana wake.


Katika barua hiyo Daudi aliandika hivi: “Umuweke Uria kwenye mustari wa mbele, pahali ambako mapigano ni makali kabisa, kisha umwache kule na kurudia nyuma kusudi apigwe, na akufe.”


Kwa hiyo basi, kwa sababu umenizarau na umemutwaa muke wa Uria wa Hiti kuwa muke wako, mauaji hayataondoka katika jamaa yako.’


Lakini Abusaloma alizidi kumusihi, na kwa mwisho mufalme akamuruhusu Amunoni na wana wake wengine waende kwenye karamu hiyo.


Nilikuwa na watoto wanaume wawili. Siku moja, walipokuwa katika mbuga, walianza kugombana. Kwa vile hakukukuwa mutu yeyote wa kuwaamua, mumoja wao akamwua mwenzake.


Basi, wakati wa saa sita za muchana, Beni-Hadadi na wale wafalme wenzake makumi tatu na wawili waliomwunga mukono walipokuwa katika mahema yao wakikunywa na kulewa, mashambulizi yakaanza.


Siku ya saba ya karamu hiyo, mufalme Ahasuero akiwa amejaa furaha kutokana na divai aliyokuwa amekunywa, akawaita matowashi saba waliomutumikia yeye mwenyewe: Mehumani, Bizita, Harbona, Bigita, Abagita, Zetari na Karkasi.


apate divai ya kumuchangamusha, mafuta ya muzeituni ya kumwangarisha, na mukate wa kumupa nguvu.


Basi, mufalme akawaita wazalishaji wale, akawauliza: “Kwa nini mumefanya hivyo? Mbona mumewaacha watoto wanaume waishi?”


Chakula ni kwa ajili ya kujifurahisha, divai inachangamusha maisha, na feza inasababisha hayo yote.


Kwenda ukule chakula chako kwa furaha, na ukunywe divai yako kwa moyo wenye kuchangamuka, maana Mungu amekwisha kukubali kazi yako.


Usiku uleule, mufalme Belsasari wa Wakaldea, aliuawa.


Watateketezwa kama kichaka cha miiba, wao wanaoikalia kulewa. Watateketezwa kama vile majani yenye kukauka.


“Mujilinde vizuri, kusudi musilemewe na kutafuta kula ulafi, kulewa na kusumbukia maisha. Kama si vile, Siku ile ya kurudia kwa Kristo itawafikia kwa rafla


Petro na mitume wengine wakajibu: “Inatupasa sisi kumutii Mungu kuliko watu!


Kumbuka kwamba mimi nimekuamuru ukuwe imara na hodari. Usiogope wala usifazaike kwa sababu mimi Yawe, Mungu wako, niko pamoja nawe popote utakapoenda.”


Walipokuwa wanajifurahisha, kumbe wanaume watenda maovu wa muji ule wakakuja wakaizunguka nyumba ile na kugonga kwa mulango. Wakamwambia muzee mwenye nyumba: “Umutoshe inje yule mwanaume aliyekuja kwako, tulale naye.”


Basi hao watu wawili wakaikaa, wakakula na kunywa pamoja. Kisha baba mukwe akamwambia: “Tafazali, ulale hapa usiku huu na kufurahi.”


Yule Mulawi na habara yake pamoja na mutumishi wake waliposimama kwenda zao, baba mukwe wake akamwambia yule Mulawi: “Sasa muchana umekwisha na magaribi imekaribia. Ulale hapa, na kufurahi. Kesho asubui utaamuka mapema kuanza safari yako ya kurudi kwako.”


Boazi alipomaliza kula na kunywa, akachangamuka. Akakwenda karibu na lundo la shayiri, akalala. Ruta akakwenda polepole akafunua miguu yake na kulala pale.


Halafu Saulo aliwaamuru watumishi wake akisema: “Museme na Daudi kwa siri na kumwambia: ‘Mufalme anapendezwa sana nawe, hata watumishi wake vilevile wote wanakupenda’. Hivyo, sasa ukubali kuwa mukwe wa mufalme.”


Saulo akamwapia kwa jina la Yawe, akisema: “Kama vile Yawe anavyoishi, hakuna azabu yoyote itakayokupata kutokana na jambo hili.”


Mufalme Saulo akamwambia: “Usiogope! Unaona nini?” Yule mwanamuke akamujibu: “Ninaona mungu akipanda toka ndani ya udongo.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ