Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




2 Samweli 13:23 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

23 Nyuma ya miaka miwili mizima, Abusaloma alikuwa na shuguli ya kuwakata kondoo wake manyoya katika muji wa Bali-Hazori, karibu na Efuraimu. Akawaalika wana wote wa mufalme.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




2 Samweli 13:23
13 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Wakati ule Labani alikuwa amekwenda kukata manyoya ya nyama wake. Hivyo Rakeli akapata nafasi ya kuiba sanamu za miungu ya baba yake.


Abusaloma alimwendea mufalme Daudi, akamwambia: “Angalia, mimi mutumishi wako ninawakata kondoo manyoya. Ninakuomba wewe mufalme pamoja na watumishi wako, muende pamoja nami, mutumishi wako.”


Ametoa sadaka ya ngombe, ya wana-ngombe wanono, na kondoo wengi, na amewaalika wana wote wa mufalme, kuhani Abiatari, na Yoabu jemadari wa makundi yako ya waaskari, lakini mutumishi wako Solomono hakualikwa.


Kwa maana leo alienda kutoa sadaka ya ngombe, wana-ngombe wanono na kondoo wengi na amewaalika wana wote wa mufalme, Yoabu jemadari wa waaskari, na kuhani Abiatari, na sasa wanakula na kunywa mbele yake, na kusema: ‘Mufalme Adonia aishi!’


Siku moja, Adonia alitoa sadaka ya kondoo, ngombe na wana-ngombe wanono kwenye Jiwe la Zoheleti, karibu na chemichemi inayoitwa Enrogeli. Akawaalika kwenye karamu ya sadaka hiyo wandugu zake wote, ni kusema wana wengine wa mufalme, na watumishi wote wa mufalme wanaokuwa wa kabila la Yuda.


Mufalme Mesha wa Moabu alikuwa mufugaji wa kondoo, na kila mwaka alilipa kodi kwa mufalme wa Israeli wana-kondoo elfu mia moja na manyoya ya kondoo wengine elfu mia moja.


Hata katika jangwa vilevile alijenga minara, akachimba visima vingi, maana alikuwa na makundi mengi ya nyama kwenye sehemu za miinuko na mabonde. Alikuwa na walimaji na watunza mizabibu kwenye milima, na katika inchi yenye mboleo maana alipenda mulimo.


Kulikuwa mutu mumoja kule katika muji wa Maoni ambaye alikuwa na biashara ya kondoo katika muji wa Karmeli. Kule Karmeli alifuga kondoo wake na kuwakata manyoya. Alikuwa tajiri sana. Alikuwa na kondoo elfu tatu na mbuzi elfu moja.


Abigaili aliporudi kwake, alimukuta Nabali akifanya karamu kubwa katika nyumba yake kama ya kifalme. Nabali alikuwa akifurahi sana ndani ya moyo maana alikuwa amelewa sana. Kwa hiyo hakumwambia neno lolote mpaka asubui.


Basi, Daudi akiwa kule katika jangwa alisikia kwamba Nabali alikuwa anawakata kondoo wake manyoya kule Karmeli.


Nimesikia kwamba unawakata kondoo wako manyoya. Ninataka ujue kwamba wachungaji wako walikuwa pamoja nasi, nasi hatukuwazuru. Tena muda wote walipokuwa pamoja nasi katika muji wa Karmeli, hawakukosa kitu chochote.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ