Siku iliyofuata, mutu mumoja kutoka kambi ya Saulo, nguo zake zikiwa zimepasuka kwa huzuni na akiwa na mavumbi juu ya kichwa, alimwendea Daudi. Alipomufikia Daudi, alijitupa uso mpaka chini mbele yake kwa heshima.
Kaka yake, Abusaloma, alipomwona, alimwuliza: “Kaka yako Amunoni amelala nawe? Tulia dada yangu. Yeye ni kaka yako. Usichunge jambo hilo ndani ya moyo wako.” Halafu, Tamari aliishi katika nyumba ya Abusaloma akiwa na huzuni na mwenye kutupiliwa.
Mordekayi alipojua yote yaliyotukia, akapasua nguo zake, akavaa nguo ya gunia, na kujitia majivu. Kisha, akapita katikati ya muji akilia kwa sauti ya uchungu.
Siku hiyohiyo, mutu mumoja wa kabila la Benjamina alikimbia kutoka mustari wa mbele wa mapigano mpaka Shilo nazo nguo zake zikiwa zimechanika na akiwa na mavumbi kwenye kichwa.