Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




2 Samweli 12:31 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

31 Halafu aliwakamata watu wa muji ule, akawaweka kwa kazi ya kutumikisha misumeno, sururu za chuma, mashoka ya chuma na kuwatumia kufanya kazi katika furu ya matofali. Hivi ndivyo alivyoitendea miji yote ya Waamoni. Kisha Daudi na watu wote walirudi Yerusalema.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




2 Samweli 12:31
10 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kisha aliwashinda Wamoabu. Aliwapanga katika mistari mateka hao, na kuwalalisha chini. Aliamuru wale waliokuwa katika mistari miwili wauawe na wale wa mustari wa tatu waachwe wazima. Hivyo, Wamoabu wakakuwa watumishi wa Daudi na wakakuwa wanamulipa kodi.


Kisha Daudi akatwaa taji ya mufalme wao kutoka juu ya kichwa chake, naye akagundua kwamba taji hiyo ilikuwa na uzito wa kilo makumi tatu na tano za zahabu na ndani yake mulikuwa jiwe la bei kali. Daudi akavikwa taji hiyo juu ya kichwa chake. Vilevile alinyanganya vitu vingi sana kutoka katika muji ule.


Halafu akakamata watu wa muji ule, nao wakafanya kazi wakitumia misumeno, sururu za chuma na mashoka ya chuma. Ni vile ndivyo alivyoitendea miji yote ya Waamoni. Kisha Daudi na watu wote wakarudi Yerusalema.


Twaa mawe makubwa, uyafiche ndani ya udongo kwenye matofali mbele ya mulango wa nyumba ya kifalme ya Tapanesi mbele ya Wayuda.


Yawe anasema hivi: Kwa sababu ya makosa matatu ya watu wa Amoni, hata kwa mane, sitageuza nia yangu. Katika vita yao kwa kupanua inchi, walipasua tumbo za wanawake wenye mimba katika inchi ya Gileadi.


Basi, nitashusha moto juu ya kuta za muji wa Raba, na kuziteketeza kabisa nyumba zake nzuri. Siku hiyo ya vita kutakuwa makelele mengi, nayo mapambano yatakuwa makali kama zoruba.


Yawe anasema hivi: Kwa sababu ya makosa matatu ya watu wa Damasiki, hata kwa mane, sitageuza nia yangu. Wamekatakata watu wa Gileadi wakitumia majembe ya mashini ya kulima.


Wengine waliuawa kwa kutupiwa mawe, wengine walikatwa vipandevipande kwa misumeno, au kuuawa kwa upanga. Walitangatanga wakivaa ngozi za kondoo au za mbuzi, wakiishi katika umasikini, wakiteswa na kutendewa vibaya.


Kisha Yoshua akarudi katika kambi kule Gilgali pamoja na Waisraeli wote.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ