Kisha, Natani akamwendea Batiseba mama ya Solomono, akamwuliza: “Haujasikia kwamba Adonia mwana wa Hagiti amejiweka kuwa mufalme na bwana wetu Daudi hana habari?
Hata hivyo, utapata mwana ambaye atatawala kwa amani kwa sababu nitamupa amani na waadui zake wote wa jirani. Jina lake litakuwa Solomono, kwa maana katika siku za utawala wake, atailetea inchi ya Israeli amani na utulivu.
Hawa ndio wana wa mufalme Daudi waliozaliwa alipokuwa Yerusalema: Muke wake Bati-Seba, binti ya Amieli, akamuzalia wana wane: Simea, Sobabu, Natani na Solomono.
Si Solomono alitenda zambi kwa sababu ya wanawake wa namna hiyo? Yeye alikuwa mufalme mukubwa kuliko wafalme wa mataifa mengine. Mungu akamupenda na akamufanya kuwa mufalme juu ya watu wote wa Israeli, hata hivyo wanawake wa mataifa mengine, wakamusukuma kutenda zambi.
Juu ya kabila la Benjamina akasema: “Hili ni kabila Yawe analopenda, nalo linakaa salama karibu naye. Yeye analinda muchana kutwa, na kukaa kati ya milima yake.”