Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




2 Samweli 12:14 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

14 Hata hivyo, kwa sababu kwa tendo lako umemuzarau kabisa Yawe, mutoto wako atakufa.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




2 Samweli 12:14
16 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kisha Natani akarudi kwake. Yawe alimupiga mutoto ambaye Batiseba muke wa Uria alimuzalia Daudi, naye akakuwa mugonjwa.


Kisha nikawaambia: “Jambo munalofanya si zuri. Haiwapasi kumwogopa Mungu wetu kwa kuzuia mataifa mengine yanayokuwa waadui zetu yasituzarau?


Ee Mungu, unajua upumbafu wangu; makosa yangu hayafichwi mbele yako.


Ee Mungu, mpaka wakati gani adui atakuchekelea? Watakufuru jina lako milele?


Heri mutu unayemwadibisha, ee Yawe, mutu unayefundisha sheria yako,


Ee Yawe, Mungu wetu, wewe uliwasikiliza; ulikuwa kwao Mungu mwenye kusamehe, ingawa uliwaazibu kwa makosa yao.


Katika hali ya sasa ninapata faida gani kuwaona watu wangu wamepelekwa katika utumwa? –Ni ujumbe wa Yawe. Hao wanaowatawala wanajitapa. Nalo jina langu linaendelea kuzarauliwa kila siku. –Ni ujumbe wa Yawe.


Kati ya mataifa yote katika ulimwengu, ni ninyi tu niliowachagua. Kwa hiyo nitawaazibu ninyi, kwa sababu ya uovu wenu wote.


Ole kwa dunia kwa ajili ya vikwazo vinavyokuwa ndani yake! Vikwazo haviwezi kosa kutokea, lakini ole kwa mutu yule anayevileta!


Kwa maana kama ilivyoandikwa katika Maandiko Matakatifu: “Kwa sababu yenu, jina la Mungu linatukaniwa katikati ya watu wa mataifa mengine.”


Lakini tunahukumiwa na kuazibiwa na Bwana kusudi tusiazibiwe pamoja na watu wa dunia hii.


Kwa maana, Bwana anamwazibu yule anayemupenda, yeye anamupiga kila mutu anayemukubali kuwa mutu wake.”


Mimi ninawaonya na kuwaazibu wote ninaowapenda. Basi ufanye nguvu, ugeuke toka katika zambi.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ