5 Mwanamuke yule akapata mimba, naye akatuma habari kwa Daudi kwamba yuko na mimba yake.
Basi, Daudi akamutumia Yoabu ujumbe: “Umutume Uria wa Hiti kwangu.” Naye Yoabu akamutuma Uria kwa Daudi.
Maana wivu wa mume unamufanya kuwa mukali kabisa; wakati atakapolipiza kisasi hana kitu cha kuhurumia.
Kama mwanaume akifanya uzinzi na muke wa mwenzake, wote wawili wanapaswa kuuawa.
“Mutu akikamatwa akilala na muke wa mutu mwingine, wote wawili, mwanaume na mwanamuke, wanapaswa kuuawa. Ndivyo mutakavyokomesha uovu huo kati yenu.