Nani alimwua Abimeleki mwana wa Yerubeseti? Si alikuwa mwanamuke mumoja katika muji wa Tebesi ambaye alitupa jiwe la kusagia kutoka kwenye ukuta nalo likamwua Abimeleki? Kwa nini basi, mulikwenda karibu na ukuta?’ Basi, wewe utamwambia hivi: ‘Hata mutumishi wako Uria wa Hiti, naye amekufa.’ ”
Yule mujumbe akamwambia Daudi: “Waadui zetu walitushinda nguvu, wakatoka inje ya miji na kutushambulia katika mbuga. Hata hivyo sisi tuliwarudisha mpaka kwenye mulango wa muji.