Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




2 Samweli 11:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Siku moja, wakati wa magaribi, Daudi aliamuka toka katika kitanda, akaenda kwenye dari ya nyumba ya kifalme. Alipokuwa anatembea kule juu, alimwona mwanamuke mumoja akioga na mwanamuke yule alikuwa muzuri sana kwa umbo.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




2 Samweli 11:2
28 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Alipokaribia Misri, Abramu akamwambia Sarai muke wake: “Ninajua kwamba wewe ni mwanamuke muzuri na wa kuvutia.


Basi, mwanamuke alipoona kwamba muti ule ni muzuri kwa chakula, unavutia macho, na kwamba unafaa kwa kupata hekima, akachuma tunda lake, akakula, akamupa mume wake aliyekuwa pamoja naye, naye vilevile akakula.


Basi, Sekemu mwana wa Hamori Muhivi, aliyekuwa mukubwa wa inchi hiyo, alipomwona Dina, akamushika, akalala naye kwa nguvu.


Kwa sababu hiyo Potifari alimupa Yosefu mamlaka juu ya mambo yake yote, naye Potifari akaacha kushugulika na chochote isipokuwa tu chakula chake mwenyewe. Yosefu alikuwa kijana muzuri na wa kupendeza.


wana wa Mungu wakaona kwamba wale wabinti za watu ni wazuri, wakawatwaa wale waliowapendeza kuwa wake zao.


Abusaloma mwana wa Daudi, alikuwa na dada yake muzuri sana aliyeitwa Tamari. Naye Amunoni, mwana mwingine wa Daudi, akamupenda sana Tamari.


Abusaloma alizaa watoto watatu wanaume pamoja na binti mumoja jina lake Tamari. Tamari alikuwa na sura nzuri.


Rekabu na Bana wana wa Rimoni wa Beroti wakaenda kwa nyumba ya Isiboseti. Walifika kule wakati wa jua kali ya muchana, Isiboseti alipokuwa anapumzika mwake.


Nimejizuiza kabisa mimi mwenyewe, macho yangu yasimwangalie binti kwa tamaa.


Uniepushe nisifuate mambo ya ovyo; unionyeshe njia yako, unipe uzima.


Uvivu ni kama usingizi muzito; mutu muvivu atateseka kwa njaa.


Mapendezi ni udanganyifu na uzuri wa uso haukawii, lakini mwanamuke anayemwogopa Yawe atasifiwa.


Usimutamani mwanamuke yule kwa uzuri wake, wala usikubali kunaswa kwa kope za macho yake.


Huyo alikuwa akitembea kwenye barabara ile, karibu na pahali mwanamuke mumoja alipoishi. Basi akashika njia inayokwenda kwa mwanamuke yule.


Nyumba za Yerusalema na nyumba za wafalme wa Yuda, ndizo nyumba zote ambazo juu ya paa zao watu walifukiza ubani kwa kutambikia makundi ya nyota, na kuitolea miungu mingine sadaka za divai, zote zitageuzwa kuwa chafu kama Tofeti.


Neno ninalowaambia katika giza, muliseme muchana kati. Vilevile neno munalosikia kwa siri, mulitangaze mukisimama juu ya paa ya nyumba.


Atakayekutiwa juu ya paa la nyumba asishuke ndani yake kwa kutwaa kitu.


Lakini mimi ninawaambia: mutu yeyote anayemwangalia mwanamuke kwa kumutamani, amekwisha kuzini naye ndani ya moyo wake.


Kesho yake karibu na saa sita ya muchana, hao watu watatu wakafika karibu na Yopa, saa ile Petro akapanda juu ya paa kwa kuomba.


“Unapojenga nyumba, jenga ukuta pembeni ya paa, kusudi usihukumiwe kama mutu akianguka kutoka huko, na kufa.


“Usimutamani muke wa mwenzako, wala nyumba yake, wala shamba lake, wala mutumwa wake au mujakazi wake, wala ngombe wake, wala punda wake, wala kitu chochote mwenzako anachokuwa nacho.”


Mwisho wa vitu vyote unakaribia kutimia. Kwa hiyo mukuwe wenye akili na waangalifu, kusudi mukuwe na uwezo wa kuomba.


Kwa maana kila kitu kinachokuwa katika dunia, kama vile tamaa ya kimwili, tamaa ya macho, na majivuno ya maisha, hivi vyote havitoki kwa Baba, lakini vinatoka katika dunia.


Waliporudi katika muji kutoka kwenye nafasi ya ibada juu ya mulima, alizungumuza na Saulo juu ya dari. Na Saulo akalala kule.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ