Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




2 Samweli 11:16 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

16 Basi, Yoabu alipokuwa akizunguka muji, alimuweka Uria pahali ambapo alijua wazi waaskari wa waadui walikuwa hodari sana.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




2 Samweli 11:16
13 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Katika barua hiyo Daudi aliandika hivi: “Umuweke Uria kwenye mustari wa mbele, pahali ambako mapigano ni makali kabisa, kisha umwache kule na kurudia nyuma kusudi apigwe, na akufe.”


Wakaaji wa muji ule walitoka katika muji wao na kupigana na Yoabu. Watumishi wamoja wa Daudi, waliuawa. Uria wa Hiti naye aliuawa vilevile.


Nani alimwua Abimeleki mwana wa Yerubeseti? Si alikuwa mwanamuke mumoja katika muji wa Tebesi ambaye alitupa jiwe la kusagia kutoka kwenye ukuta nalo likamwua Abimeleki? Kwa nini basi, mulikwenda karibu na ukuta?’ Basi, wewe utamwambia hivi: ‘Hata mutumishi wako Uria wa Hiti, naye amekufa.’ ”


Abeneri aliporudi Hebroni, Yoabu alimupeleka pembeni kwenye mulango sawa vile anataka kuzungumuza naye kwa siri. Hapo Yoabu akamukata Abeneri katika tumbo kwa sababu Abeneri alikuwa amemwua ndugu yake Asaeli, na Abeneri akakufa.


“Zaidi ya hayo, unajua vilevile yale Yoabu mwana wa Zeruya aliyonitendea, jinsi alivyowatendea majemadari wawili wa waaskari wa Israeli, Abeneri mwana wa Neri, na Amasa mwana wa Yeteri. Aliwaua wakati wa amani akitaka kulipiza kisasi kwa mauaji waliyofanya wakati wa vita. Aliwaua watu wasiokuwa na kosa, nami nikabeba lazima ya kifo cha watu wale kwa ajili ya vitendo vyake.


Yehu akawaandikia barua ingine akiwaambia: “Ikiwa kweli muko tayari kufuata maagizo yangu, mulete hapa Yezereheli vichwa vya wana wa bwana wenu nivipate kesho kwa wakati kama huu.” Wana makumi saba wa mufalme Ahabu waliishi kwa viongozi wa Samaria, ambao walikuwa walezi wao.


Mutawala akisikiliza mambo ya uongo, wakubwa wake wote watakuwa waovu.


Efuraimu ameteswa, haki zake zimetwaliwa; maana alikusudia kufuata mambo isiyokuwa na maana.


Petro na mitume wengine wakajibu: “Inatupasa sisi kumutii Mungu kuliko watu!


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ