14 Asubui yake, Daudi alimwandikia Yoabu barua, akamupa Uria aipeleke kwa Yoabu.
Kwa nini basi, umezarau neno langu mimi Yawe na kufanya uovu huu mbele yangu? Umemwua Uria wa Hiti kwa upanga, ukamukamata muke wake kuwa muke wako. Umewatumia Waamoni kwa kumwua Uria katika vita!
Lakini nani anayeona makosa yake mwenyewe? Ee Mungu, unisamehe makosa nisiyoyajua.
Enyi watu, mutumainie Mungu siku zote; mumufungulie yanayokuwa ndani ya moyo wenu. Yeye ndiye kimbilio letu.
Moyo wa mutu ni mudanganyifu kuliko vitu vyote; hauwezi kuponyeshwa, hakuna anayeweza kuuelewa!