Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




2 Samweli 11:11 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

11 Uria alimujibu Daudi: “Sanduku la Agano, pamoja na waaskari wote wa Israeli na Yuda wanakaa kwenye vibanda katika vita. Bwana wangu Yoabu na watumishi wake wote wamepiga kambi katika mbuga. Basi ni vizuri mimi niende nikule na kunywa na kulala na muke wangu? Ninaapa kwamba, kama vile unavyoishi, sitafanya kitu cha namna ile.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




2 Samweli 11:11
19 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Daudi aliposikia kwamba Uria hakwenda kwake, Daudi akamwuliza Uria: “Wewe umetoka safari, kwa nini haukuenda kwako?”


Mufalme akamwuliza: “Haukupatana na Yoabu katika jambo hili?” Yule mwanamuke akasema: “Kama vile unavyoishi mwenyewe bwana wangu mufalme, mutu hawezi kupita pembeni juu ya jambo ulilosema bwana wangu mufalme. Yoabu yule mutumishi wako ndiye aliyenituma. Ni yeye aliyeniambia maneno yote haya niliyokuambia mimi mujakazi wako.


Daudi akamwambia Abisayi: “Sasa, Seba mwana wa Bikiri, atatuletea taabu kuliko Abusaloma. Twaa watumishi wangu, umufuate Seba kusudi asiingie kwenye miji yenye kuta na kuponyoka tusimwone tena.”


mufalme Daudi akamwambia nabii Natani: “Angalia, mimi ninakaa katika nyumba iliyojengwa na miti ya mierezi, lakini Sanduku la Mungu linakaa ndani ya hema.”


Tangu siku ile nilipowatoa Waisraeli katika inchi ya Misri mpaka hivi leo sijaishi kwenye nyumba. Nimetembea kila pahali nikiwa ninakaa katika hema.


Musa akawajibu watu wa makabila ya Gadi na Rubeni: Munataka kubaki hapa wakati wandugu zenu Waisraeli wanakwenda kwa vita?


Basi kama mimi ninayekuwa Bwana na Mwalimu wenu nimewanawisha miguu, ninyi vilevile munapaswa kunawishana miguu.


Kama tunaendelea kuvumilia, tutatawala pamoja naye vilevile. Kama tunamukana, naye atatukana vilevile.


Hana akamwambia: “Ee bwana wangu, kama vile unavyoishi, bwana wangu, mimi ni yule mwanamuke aliyekuwa anasimama mbele yako akimwomba Yawe.


Saulo akamwambia kuhani Ahiya: “Ulete hapa Sanduku la Agano la Mungu.” (Wakati huo Sanduku la Agano la Mungu lilikuwa pamoja na Waisraeli.)


Saulo alipomwona Daudi akienda kupigana na yule Mufilistini Goliati, alimwuliza Abeneri, jemadari wa kundi lake: “Abeneri, huyu ni kijana wa nani?” Abeneri alijibu: “Ee Mufalme, ninaapa kwa jina lako, mimi sijui.”


Daudi akaapa vilevile: “Hakika baba yako anajua vizuri kwamba nimepata kukubaliwa mbele yako. Anafikiri kukuficha juu ya jambo hili kusudi usihuzunike atakapolitenda. Lakini kweli, kama Yawe anavyoishi na kama wewe mwenyewe unavyoishi, kati yangu na lufu kuna hatua moja tu!”


Sasa bwana wangu, kama vile Yawe anavyoishi na kama vile unavyoishi, unaona kwamba Yawe amekuzuia kulipiza kisasi kwa kumwanga damu na hivyo upate kuwa na kosa. Uwaache waadui zako na wale wote wanaokutakia mabaya wakuwe wapumbafu kama Nabali.


Kwa hiyo, walituma watumishi kule Shilo, nao wakalileta Sanduku la Agano la Yawe wa majeshi ambaye anatawala juu ya makerubi. Wale wana wawili wa Eli, Hofuni na Finehasi walikuja pamoja na lile Sanduku la Agano la Mungu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ