Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




2 Samweli 10:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

8 Waamoni walitoka na kujipanga tayari kwa vita kwenye mulango wa muji wa Raba, muji wao mukubwa; nao Waaramu kutoka Zoba na Rehobu na watu kutoka Tobu na Maka walijipanga katika mbuga.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




2 Samweli 10:8
13 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Waamoni walipoona kwamba wamemuchukiza Daudi, walijilipia waaskari wa miguu wa Waaramu elfu makumi mbili kutoka Beti-Rehobu na Zoba, waaskari elfu kumi na mbili kutoka Tobu, na mufalme Maka akiwa na waaskari elfu moja.


Naye Daudi aliposikia habari zile, alimutuma Yoabu kwenda na kundi lote la waaskari mashujaa.


Yoabu alipoona kwamba ilimupasa kupigana kwa upande wa mbele na nyuma, alichagua waaskari wamoja Waisraeli hodari zaidi, akawapanga mbele ya Waaramu.


Elifeleti mwana wa Ahasibayi wa Maka; Eliamu mwana wa Ahitofeli wa Gilo;


Nyuma ya Daudi kufanya mauaji kule Zoba, Resoni alikusanya watu, naye mwenyewe akakuwa kiongozi wao. Basi, wakaenda Damasiki, wakakaa kule na kumufanya Resoni mufalme wa Damasiki.


Walikopesha magari elfu makumi tatu na mawili, na mufalme wa Maka na waaskari wake akakuja na kupiga kambi karibu na Medeba. Waamoni walikusanyika toka kwenye miji yao yote, wakajiweka tayari kwa vita.


Waamoni wakatoka na kujipanga kwenye mulango wa muji, wakati wale wafalme waliokuja walikuwa peke yao kwenye mbuga.


walimwendea Gedalia kule Misipa. Watu hao walikuwa Isimaeli mwana wa Netania, Yohana na Yonatani wana wa Karea, Seraya mwana wa Tanumeti, nao wana wa Efai kutoka muji Netofa, na Yezania wa muji wa Makati; wote pamoja na watu wao.


Basi, watu hao wakaenda na kupeleleza inchi toka jangwa la Sini mpaka Rehobu, karibu na njia ya kuingilia Hamati.


Eburoni, Rehobu, Hamoni, Kana mpaka Sidona muji mukubwa.


Watu wa kabila la Aseri hawakuwafukuza wakaaji wa miji ya Ako, Sidona, Alabu, Akizibu, Helba, Afika na Rehobu.


Basi, Yefuta akawakimbia wandugu zake akaenda kuishi katika inchi ya Tobu. Kule watu wa ovyo wakakusanyika kujiunga naye, wakamufuata katika safari zake za mashambulio.


Wakati vita ilipopamba moto, wazee wa Gileadi wakaenda kumuleta Yefuta kutoka inchi ya Tobu,


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ