Daudi alipopata habari, aliwakusanya pamoja waaskari wote wa Israeli, akavuka muto Yordani na kwenda mpaka Helamu. Nao Waaramu walijipanga tayari kwa vita na Daudi, wakaanza kupigana naye.
Daudi akamushinda vilevile Hadadezeri mufalme wa Zoba, inchi iliyokuwa karibu na Hamati, alifanya hivyo wakati alipokuwa akienda kujisimamishia nguzo ya ukumbusho kwenye sehemu za muto Furati.
Lakini Waaramu walipoona kwamba wameshindwa na Waisraeli, wakatuma wajumbe waende kuwaleta Waaramu wengine waliokuwa ngambo ya muto Furati wakiongozwa na Sofaki, jemadari wa jeshi la Hadadezeri.