2 Samweli 10:12 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
12 Lakini ujipe moyo! Tupigane kama wanaume kwa ajili ya watu wetu na kwa ajili ya miji ya Mungu wetu. Naye Yawe atutendee lile analoona ni jema kwake.”
“Muwe imara na hodari. Musiogope wala musifazaike mbele ya mufalme wa Asuria au majeshi yake maana tunayekuwa naye ni mukubwa kuliko anayekuwa na Saniharibu.
Nilipoona kwamba watu walikuwa na hofu nikawaambia wakubwa, wasimamizi na watu wote kwa jumla: “Musiwaogope hata kidogo. Mukumbuke Bwana anayekuwa mukubwa na wa kutisha, basi mupigane kwa ajili ya wandugu zenu, wana wenu, wabinti zenu, wake zenu na nyumba zenu.”
“Kwenda uwakusanye pamoja Wayuda wote wanaokuwa katika muji wa Susani. Mufunge, musikule wala musikunywe kwa siku tatu, usiku na muchana, kwa ajili yangu. Na mimi na wajakazi wangu tutafanya vile vile. Kisha, nitamwendea mufalme, ingawa ni kinyume cha sheria. Kama ni kuuawa, niuawe.”
Muchunguze vilevile kama inchi yenyewe ni tajiri au masikini, ina miti au haina. Mukuwe na mioyo ya ushujaa na munaporudi mulete matunda ya inchi hiyo. Ilikuwa ni wakati zabibu zinapoanza kuivya.
Mukuwe imara na hodari, wala musiwaogope au kutishwa nao, maana Yawe, Mungu wenu, ndiye anayekwenda pamoja nanyi. Yeye hataacha kuwasaidia na hatawatupa.”
Kisha Musa akamwita Yoshua, akamwambia mbele ya watu wote wa Israeli: “Ukuwe imara na hodari, maana wewe utawaongoza watu hawa kwenda kurizi inchi ambayo Yawe aliwaahidi babu zao, nawe utawapatia wairizi.
Kumbuka kwamba mimi nimekuamuru ukuwe imara na hodari. Usiogope wala usifazaike kwa sababu mimi Yawe, Mungu wako, niko pamoja nawe popote utakapoenda.”
Yonatani akamwambia yule kijana aliyemubebea silaha: “Kuja, tuende kwenye ile kambi ya hawa watu wasiotahiriwa. Labda Yawe atatusaidia, maana Yawe haokoi kwa kutegemea wingi au uchache wa watu.”
Sasa, enyi Wafilistini, mujipe moyo. Mukuwe hodari kusudi musipate kuwa watumwa wa Waebrania kama wao walivyokuwa watumwa wetu. Mukuwe hodari kama wanaume na kupigana.”