Kwa hiyo, nilikwenda karibu naye na kumwua, kwa sababu nilikuwa na uhakika kwamba akianguka chini, hataweza kuishi zaidi. Lakini taji iliyokuwa juu ya kichwa chake na kikomo kilichokuwa kwenye mukono wake, vyote nimekuletea wewe, bwana wangu.”
Kwa hiyo Saulo akamwambia mutu aliyemubebea silaha: “Chomoa upanga wako unichome nikufe, kusudi watu hawa wasiotahiriwa wasikuje kunichekelea.” Lakini yule aliyemubebea silaha hakutaka kufanya vile; aliogopa sana. Halafu, Saulo alitwaa upanga wake mwenyewe akauangukia.
Halafu Saulo akamwambia mutu aliyemubebea silaha: “Chomoa upanga wako unichome nikufe, kusudi watu hawa wapagani wasikuje kunichoma upanga na kunichekelea.” Lakini yule aliyemubebea silaha hakusubutu kwa sababu aliogopa sana. Kwa hiyo, Saulo alitwaa upanga wake mwenyewe, na kuuangukia.