Daudi akamwambia: “Uniambie jinsi mambo yalivyokuwa kule.” Yule mutu akamujibu: “Watu wetu wameyakimbia mapigano na wengi kati yetu wameuawa. Zaidi ya hayo, Saulo na mwana wake Yonatani vile vile wameuawa.”
Yule kijana akamujibu: “Kwa bahati, nilikuwa juu ya mulima Gilboa. Nilimwona Saulo akiegemea mukuki wake na magari ya waaskari wapanda-farasi ya waadui zake yalikuwa yanamusonga sana.