Basi, niliunyoosha mukono wangu kwa kukuazibu. Nilipunguza chakula chako, nikakuachilia kwa waadui zako, wabinti za Wafilistini ambao walipata haya sana juu ya tabia yako chafu sana.
Haukufanya hivyo mbele uovu wako haujafichuliwa. Sasa umekuwa kama Sodoma. Umekuwa kitu cha kuchekelewa mbele ya wabinti za Edomu na jirani zake wote, na wabinti za Wafilistini jirani zako ambao walikuchukia.
Yefuta alipokuwa anarudi kwake kule Misipa, binti yake akatoka kuja kumupokea akicheza na kupiga matari. Binti huyo alikuwa ndiye mutoto wake wa pekee. Yefuta hakukuwa na mutoto mwingine mwanaume wala mwanamuke.
Hapo roho wa Yawe akamushika Samusoni kwa nguvu, naye akaenda muji Askeloni, akawaua watu makumi tatu, kisha akatwaa nguo zao za sikukuu, akawapa wale waliotegua kitendawili chake. Halafu akaondoka, akaenda kwa nyumba kwa wazazi wake akiwa na hasira kali.
Yonatani akamwambia yule kijana aliyemubebea silaha: “Kuja, tuende kwenye ile kambi ya hawa watu wasiotahiriwa. Labda Yawe atatusaidia, maana Yawe haokoi kwa kutegemea wingi au uchache wa watu.”
Daudi akawauliza wale waliokuwa karibu naye: “Mutu atakayemwua Mufilistini huyu na kuikomboa Israeli kutokana na haya hii atafanyiwa nini? Ni nani huyu Mufilistini, mutu mupagani, anayesubutu kuwatukana waaskari wa Mungu Mwenye Uzima?”
Mimi mutumishi wako nimekwisha kuua simba wengi na dubu wengi. Sasa, hata yule Mufilistini mupagani, ambaye amewatukana waaskari wa Mungu Mwenye Uzima, atakuwa kama wao.
Waaskari walipokuwa wanarudi kwenye nyumba, pamoja na Daudi kisha kumwua yule Mufilistini, wanawake kutoka kila muji katika Israeli walitoka kwenda kumupokea mufalme Saulo. Wanawake nao walikuwa wanaimba nyimbo za furaha, wakipiga matari na vinubi.
Halafu Saulo akamwambia mutu aliyemubebea silaha: “Chomoa upanga wako unichome nikufe, kusudi watu hawa wapagani wasikuje kunichoma upanga na kunichekelea.” Lakini yule aliyemubebea silaha hakusubutu kwa sababu aliogopa sana. Kwa hiyo, Saulo alitwaa upanga wake mwenyewe, na kuuangukia.
Wafilistini walizipeleka zile sanamu tano za zahabu na za majipu kwa Yawe zikiwa sadaka ya malipo ya makosa yao, sanamu moja kwa ajili ya muji mumoja, muji wa Asidodi, muji wa Gaza, muji wa Asikeloni, muji wa Gati na kwa muji wa Ekuroni.