Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




2 Samweli 1:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Siku iliyofuata, mutu mumoja kutoka kambi ya Saulo, nguo zake zikiwa zimepasuka kwa huzuni na akiwa na mavumbi juu ya kichwa, alimwendea Daudi. Alipomufikia Daudi, alijitupa uso mpaka chini mbele yake kwa heshima.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




2 Samweli 1:2
25 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kwa siku ya tatu, Abrahamu aliinua macho akaona pahali pale kwa mbali.


Basi, Rubeni aliporudi kwenye lile shimo, hakumwona Yosefu tena, kwa hiyo akararua nguo zake kwa huzuni,


Halafu Yakobo akararua nguo zake kwa huzuni, akavaa nguo ya gunia katika kiuno. Akamulilia mwana wake kwa muda wa siku nyingi.


Wakamujibu: “Mutumishi wako, baba yetu, yuko salama na angali muzima.” Kisha wakainama kwa heshima.


Daudi akamwambia: “Unatoka wapi?” Naye akamwambia: “Nimetoroka kutoka katika kambi ya Waisraeli.”


Basi, Tamari alijipakaa majivu kwenye kichwa, akapasua kanzu yake, akaweka mikono yake juu ya kichwa, halafu akaondoka akiwa analia kwa sauti.


Huyo mwanamuke kutoka Tekoa akaenda kwa mufalme, akainama uso mpaka chini mbele ya mufalme, akamwambia: “Ee mufalme, unisaidie.”


Daudi alipofika kwenye kichwa cha mulima, nafasi ya kumwabudia Mungu, mutu mumoja jina lake Husai kutoka inchi ya Arki alikuja kwa kumupokea, nguo zake zikiwa zimepasuka na juu ya kichwa chake kuna mavumbi.


Arauna alipoangalia upande wa chini alimwona mufalme akimusogelea pamoja na watumishi wake, naye akatoka, akaenda na kuinama uso mpaka chini mbele ya mufalme.


Yule mutu aliyekuja kuniambia kwamba Saulo amekufa, akizani kwamba ananiletea habari njema, nilimukamata na kumwua kule. Hivyo ikakuwa ndiyo zawadi niliyomupa kutokana na habari yake.


“Kwenda uwakusanye pamoja Wayuda wote wanaokuwa katika muji wa Susani. Mufunge, musikule wala musikunywe kwa siku tatu, usiku na muchana, kwa ajili yangu. Na mimi na wajakazi wangu tutafanya vile vile. Kisha, nitamwendea mufalme, ingawa ni kinyume cha sheria. Kama ni kuuawa, niuawe.”


Kisha siku tatu ya kufunga kwake, Esteri akavaa nguo zake za kimalkia, akaenda kusimama katika kiwanja cha ndani cha nyumba ya mufalme, kuelekea chumba cha mufalme. Mufalme alikuwa mule ndani akiikaa katika kiti chake cha kifalme, kuelekea mulango wa nyumba ya mufalme.


Mumwambie Mungu: “Matendo yako ni ya ajabu! Kwa nguvu yako kubwa waadui zako wanaishiwa nguvu.


Wataomboleza kwa uchungu wa moyo juu yako, na kulia kwa uchungu mukubwa; watajitupia mavumbi juu ya vichwa vyao na kugaagaa kwenye majivu.


Nyuma ya siku mbili atatupatia tena uzima. Nyuma ya siku tatu atatufufua kusudi tuweze kuishi pamoja naye.


Munapasua nguo zenu kwa kuonyesha huzuni, lakini inafaa mioyo yenu ipasuke vilevile. Murudilie Yawe, Mungu wenu. Yeye amejaa huruma na rehema, hakasiriki upesi, ni mwingi wa wema, na tayari kubadilisha nia zake kusudi asiazibu.


Kwa maana, kama vile Yona alivyobaki ndani ya tumbo la samaki mukubwa kwa muda wa siku tatu, muchana na usiku, ndivyo vilevile Mwana wa Mutu atakavyobaki ndani ya udongo kwa muda wa siku tatu, muchana na usiku.


Tangia wakati ule Yesu akaanza kuwaambia wanafunzi wake waziwazi kwamba ni sherti kwake kwenda Yerusalema, ateswe kule na wasimamizi wa watu, wakubwa wa makuhani na walimu wa Sheria, auawe, na kwa siku ya tatu kisha kufa kwake, atafufuka.


Yoshua akapasua nguo yake, yeye pamoja na wazee wa Israeli. Wakajitupa chini ya Sanduku la Yawe mpaka magaribi; wakajitia mavumbi juu ya vichwa vyao.


Angalia, nitakupa watu wa kikundi chenye kuabudu Shetani, ndio wale wasema uongo wanaojidai kwamba wao ni Wayuda, lakini ni wadanganyifu. Hakika nitawalazimisha kupiga magoti mbele yako, nao watajua ya kuwa mimi ninakupenda.


Yule kijana alipokwisha kuondoka, Daudi akasimama na kutoka pahali alipojificha karibu na lundo la mawe. Aliinama chini kwa heshima mara tatu mbele ya Yonatani. Wote wawili, Daudi na Yonatani, wakakumbatiana na kulia. Daudi alikuwa na uchungu zaidi kuliko Yonatani.


Abigaili alipomwona tu Daudi, akashuka mara moja kutoka juu ya punda wake, na kuinama mbele ya Daudi mpaka uso wake ukagusa chini.


Siku hiyohiyo, mutu mumoja wa kabila la Benjamina alikimbia kutoka mustari wa mbele wa mapigano mpaka Shilo nazo nguo zake zikiwa zimechanika na akiwa na mavumbi kwenye kichwa.


Yule mutu akamwambia Eli: “Mimi nimetoka kwenye vita; nimekimbia kutoka katika vita leo.” Eli akamwuliza: “Mwana wangu, mambo yalikuwa namna gani kule?”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ