Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




2 Mambo ya Siku 7:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Waisraeli wote walipoona moto ukishuka kutoka mbinguni na utukufu wa Yawe katika nyumba, wakainama nyuso zao zikifika mpaka chini. Wakamwabudu na kumushukuru Yawe wakisema: “Yeye ni muzuri. Wema wake unadumu milele.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




2 Mambo ya Siku 7:3
26 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Watu walipoona hivyo, walianguka uso mpaka chini na kusema: “Yawe ndiye Mungu! Yawe ndiye Mungu!”


Mumushukuru Yawe! Yeye ni muzuri, wema wake unadumu milele!


Pamoja nao kulikuwa Hemani na Yedutuni na wale wote waliochaguliwa, waliotajwa majina yao, kwa kumushukuru Yawe kwa sababu wema wake unadumu milele.


Kisha, mufalme Daudi akawaambia wote waliokusanyika: “Mumusifu Yawe, Mungu wenu.” Na wote waliokusanyika wakamutukuza Yawe, Mungu wa babu zao, wakainama mbele yake na kumwabudu Yawe na kumutolea mufalme Daudi heshima.


Kisha mufalme Yosafati akainama uso mpaka chini pamoja na watu wote wa Yuda na wakaaji wa Yerusalema na kumwabudu Yawe.


Nyuma ya kushauriana na watu, mufalme akachagua waimbaji kwa kumwimbia Yawe wavae nguo zao takatifu kisha watangulie mbele ya jeshi, wakiimba: “Mumushukuru Yawe, maana wema wake unadumu milele!”


Watu wote waliokuwa mule wakashiriki katika ibada. Waimbaji wakaendelea na kuimba, na baragumu zikaendelea kupigwa mpaka wakati shuguli za utoaji wa sadaka hiyo ya kuteketeza kwa moto ilipokamilika.


Kisha, mufalme Hezekia pamoja na watu wote waliokuwa pale wakainama, kwa kumwabudu Yawe.


Kisha mufalme Hezekia na viongozi wakawaambia Walawi wamusifu Yawe kwa nyimbo ambazo mufalme Daudi na nabii Asafu walizotunga. Basi, watu wote wakamutukuza Mungu kwa furaha, na kuinama uso mpaka chini.


Waimbaji na wapiga baragumu wote pamoja walitoa sauti kwa pamoja na matoazi na vyombo vingine vya muziki, wakimusifu Yawe wakiimba: “Yeye ni muzuri. Wema wake unadumu milele.” Wakati ule nyumba ya Yawe ikajazwa na wingu.


Wakaimba kwa kupokezana, wakimusifu na kumutukuza Yawe: “Yeye ni muzuri, wema wake kwa Waisraeli unadumu milele.” Watu wote walipaza sauti kwa nguvu zao zote, wakamusifu Yawe kwa sababu ya kuanza kujenga musingi wa nyumba ya Yawe.


Yawe ni muzuri! Wema wake unadumu milele, na uaminifu wake kwa vizazi vyote.


Lakini wema wa Yawe unadumu milele, kwa wale wote wanaomwabudu; na haki yake inadumu vizazi vyote,


Haleluia! Mumushukuru Yawe kwa sababu ni muzuri! Wema wake unadumu milele!


Mumushukuru Yawe kwa sababu ni muzuri! Wema wake unadumu milele!


Mumushukuru Yawe, kwa sababu ni muzuri! Wema wake unadumu milele!


Mukuje tuiname chini na kumwabudu; tumupigie magoti Yawe, Muumba wetu!


Watu wakaamini. Na waliposikia kwamba Yawe amekuja kuwasaidia Waisraeli na kwamba ameyaona mateso yao, wote wakainamisha vichwa vyao na kumwabudu.


Nitakumbusha mema ya Yawe, sifa za Yawe, matendo yake yote kwetu, mambo mazuri aliyowatendea Waisraeli, rehema yake, na wingi wa wema wake.


sauti za arusi na za furaha, sauti za waimbaji wakati wanaleta sadaka za shukrani katika nyumba ya Yawe. Wataimba hivi: Mumushukuru Yawe wa majeshi kwa sababu Yawe ni muzuri, kwa maana wema wake unadumu milele. Nitairudishia inchi hii hali yake ya zamani. –Ni Yawe anayesema.


Yawe akawasha moto ukaiteketeza sadaka ya kuteketezwa na mafuta yaliyokuwa juu ya mazabahu. Watu wote walipoona huo moto wakapiga vigelegele na kuinama uso mpaka chini.


Hapo, Musa na Haruni wakaanguka uso mpaka chini mbele yao.


Lakini Musa na Haruni wakajitupa uso mpaka chini na kusema: Ee Yawe unayekuwa asili ya uzima wa wanadamu wote. Mutu mumoja akikukosea, utakasirikia watu wote pamoja?


Yeye anawasikilia wale wanaomwogopa huruma kwa vizazi vyote.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ