Hezekia akajitia moyo, akajenga upya ukuta wote uliokuwa umebomoka, na juu yake akajenga minara. Upande wa inje, akajenga ukuta mwingine wa pili, na akaiimarisha uwanja wa Milo katika muji wa Daudi. Zaidi ya hayo akatengeneza silaha na ngao kwa wingi.
Mufalme ataomboleza, mukubwa atakata tamaa na watu watatetemeka kwa hofu. Nitawatendea kufuatana na mienendo yao, nitawahukumu kama nilivyowahukumu wengine. Halafu watatambua kwamba mimi ni Yawe.
Haya ndiyo majina ya wakubwa wa mashujaa wa Daudi, ambao pamoja na watu wengine wote wa Israeli, walimwunga mukono kwa pamoja kusudi akuwe mufalme, sawa na neno Yawe alilotoa juu ya Waisraeli.
Aliweka majeshi katika miji yote ya inchi ya Yuda yenye kuta, na katika maeneo mengine ya Yuda akaweka waaskari walinzi, na katika miji ya Efuraimu ambayo baba yake Asa aliiteka.
Kisha Ahazia akakufa kama vile Yawe alivyomwambia nabii wake Elia. Na kwa sababu Ahazia hakukuwa na mutoto mwanaume, Yoramu akakuwa mufalme kwa pahali pake, katika mwaka wa pili wa utawala wa Yehoramu mwana wa Yosafati, mufalme wa Yuda.