Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




1 Yoane 5:9 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

9 Kama tunakubali ushuhuda wa wanadamu, ushuhuda wa Mungu ni wenye maana zaidi, na ni huu ndio ushuhuda Mungu aliotoa juu ya Mwana wake.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




1 Yoane 5:9
13 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Naye alipokuwa angali akisema, wingu lenye kuangaza likawafunika, na sauti ikasikilika toka katikati ya lile wingu ikisema: “Huyu ni Mwana wangu mupendwa, ninapendezwa naye sana. Mumusikilize!”


Lakini kama nikiyatenda, hata ikiwa hamuniamini mimi, basi mwamini matendo yangu, kusudi mupate kujua kabisa kwamba mimi na Baba ni mumoja, yeye ni ndani yangu, nami ndani yake.”


Munachunguza Maandiko Matakatifu, kwa maana munazani kuwa ndani yao mutapata uzima wa milele. Maandiko hayo ndiyo yanayonishuhudia,


Kwa maana amekwisha kupanga siku atakapohukumu dunia kwa haki, kwa njia ya mutu mumoja, yule aliyemuweka kwa kazi ile. Naye amehakikisha mambo hayo kwa kumufufua mutu yule.”


Na sisi ni washuhuda wa mambo hayo, naye Roho Mutakatifu ambaye Mungu aliwapa wale wanaomutii, anayashuhudia vilevile.”


Mungu vilevile alihakikisha ushuhuda wao kwa njia ya maajabu, ya miujiza mbalimbali, na ya vitambulisho, na kwa njia ya zawadi za Roho Mutakatifu alizowapa watu kama anavyopenda.


Basi kuna mambo mawili, ahadi na kiapo, yasiyoweza kubadilika, na kuelekea hayo, Mungu hawezi kusema uongo. Kwa hivi, sisi tuliomukimbilia tunatiwa moyo sana na kushika kwa nguvu tumaini tulilowekewa.


Yule anayemwamini Mwana wa Mungu yuko na ushuhuda huu ndani yake. Lakini yule asiyemwamini Mungu, amemufanya Mungu kuwa mwongo, maana hakuaminia ushuhuda Mungu aliotoa juu ya Mwana wake.


Roho, maji na damu, nao watatu wanapatana kwa ushuhuda mumoja.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ