Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




1 Yoane 5:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Kwa maana kumupenda Mungu ni kutii amri zake. Na amri zake si ngumu,

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




1 Yoane 5:3
26 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Yeye hakumwasi Yawe wala hakuacha kumufuata, lakini alishika amri ambazo Yawe alimupa Musa.


Ahadi yako ni hakika kabisa, nami mutumishi wako ninaipenda.


Nitaishi katika uhuru kamili, maana ninashugulika na kanuni zako.


Lakini ninawatendea mema maelfu ya wale wanaonipenda na kushika amri zangu.


Njia zake ni za kupendeza, zote zinaelekea kwenye amani.


Nilimwomba Yawe, Mungu wangu, na kuitikia zambi, nikisema: Ee Bwana, wewe ni Mungu mukubwa na wa kuogopesha. Wewe unashika agano lako na kutenda mema kwa wanaokupenda na kuzitii amri zako.


Mungu amekuonyesha yanayokuwa mema, ewe mwanadamu; kitu Yawe anachotaka kwako ni hiki: kutenda mambo ya haki, kupenda kuwa na huruma, na kuishi kwa unyenyekevu mbele ya Mungu wako.


Wanafunga mizigo mizito na kuibebesha watu wengine kwa mabega, lakini wao wenyewe hawafikiri hata kidogo juu ya namna ya kuwasaidia kuibeba.


“Kama munanipenda, mutashika amri zangu.


Kama mukishika amri zangu, mutakaa katika upendo wangu, kama vile mimi nilivyoshika amri za Baba yangu na kukaa katika upendo wake.


Ninyi ni warafiki zangu, kama mukifanya sawa ninavyowaagiza.


Basi Sheria yenyewe ni takatifu na amri ni takatifu, ya haki na nzuri.


Ndani ya roho yangu ninapendezwa na Sheria ya Mungu,


Lakini ninawatendea mema maelfu ya wale wanaonipenda na kushika amri zangu.


Basi, mujue kwamba Yawe, Mungu wenu, ndiye Mungu. Yeye ni Mungu mwaminifu, anayeshika agano lake na kutenda mema kwa vizazi vingi vya wale wanaomupenda na kushika amri zake.


Sasa hili ndilo agano nitakalofanya na watu wa ufalme wa Israeli katika siku zile: nitawawezesha kuchunga sheria zangu ndani ya mafikiri yao, nikiziandika ndani ya mioyo yao. Ni Bwana wetu Mungu anayesema hivyo. Nitakuwa Mungu wao, nao watakuwa watu wangu.


Sisi tunatambua kwamba tunamujua Mungu ikiwa tunashika amri zake.


Na upendo ni kuishi katika kutii amri za Mungu. Hii ndiyo ile amri muliyoisikia tangu mwanzo: muishi katika upendo.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ