2 Hii ndiyo namna tunavyojua kwamba tunawapenda watoto wa Mungu: kwa kumupenda Mungu na kushika amri zake.
Amri ninawapa ni kwamba mupendane ninyi kwa ninyi.
Sisi tunatambua kwamba tunamujua Mungu ikiwa tunashika amri zake.
Lakini yule anayetii neno la Mungu yuko na upendo kamili wa Mungu ndani yake. Hili ndilo jambo linalotuonyesha kwamba sisi tunaungana na Mungu:
Sisi tunajua kwamba tumeponyoka lufu na kupata uzima kwa sababu tunawapenda wandugu zetu. Mutu asiyekuwa na upendo ni kama mufu.
Basi hii ndiyo amri tuliyopewa na Kristo: yule anayemupenda Mungu anapaswa kumupenda ndugu yake vilevile.