Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




1 Yoane 5:10 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

10 Yule anayemwamini Mwana wa Mungu yuko na ushuhuda huu ndani yake. Lakini yule asiyemwamini Mungu, amemufanya Mungu kuwa mwongo, maana hakuaminia ushuhuda Mungu aliotoa juu ya Mwana wake.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




1 Yoane 5:10
22 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Nani basi, anayeweza kuhakikisha kwamba mimi ni mwongo na kuonyesha kwamba maneno yangu si kweli?


Yawe ni rafiki ya wale wanaomwabudu; yeye anawajulisha agano lake.


Maana waovu ni chukizo kwa Yawe, yeye anawafanya watu wa usawa kuwa warafiki zake.


Ni nani aliyeamini mambo tuliyoyasikia? Mukono wa Mungu umefunuliwa kwa ajili ya nani?


Kwa nini mateso yangu hayaishi? Mbona kidonda changu hakiponi nacho hakitaki kutunzwa? Kama vile kijito chenye kukaukakauka, kisivyoweza kutumainiwa, ndivyo wewe umekuwa kwangu!


Mungu si mutu, hata aseme uongo, wala si mwanadamu, hata abadilishe nia yake! Ataahidi kitu na asikifanye, au kusema kitu asikitimize?


Kwa maana Mungu alipenda sana ulimwengu hata kumutoa Mwana wake wa pekee, kusudi kila mutu anayemwamini asipotee, lakini apate uzima wa milele.


Anayemwamini Mwana hahukumiwi, lakini asiyemwamini amekwisha kuhukumiwa, kwa sababu hakumwamini Mwana wa pekee wa Mungu.


Yeyote anayekubali ushuhuda wake anahakikisha kama Mungu ni mwenye ukweli.


Ninyi hamuchungi neno lake ndani yenu, kwa sababu ninyi hamumwamini yule aliyetumwa naye.


Filipo akamwambia: “Kama unaamini kwa moyo wako wote, unaweza kubatizwa.” Yule mukubwa akamujibu: “Ninaamini kwamba Yesu Kristo ni Mwana wa Mungu.”]


Roho huyo mwenyewe anahakikisha ndani ya roho zetu kwamba sisi ni watoto wa Mungu.


Mimi ninataka kusema hivi: mwana anayepaswa kurizi mali ya baba yake anatendewa kama mutumwa kwa muda wote anapokuwa angali mudogo, ijapokuwa yeye ndiye kweli mwenyeji wa mali yote.


Mungu alituma Roho wa Mwana wake ndani ya moyo wetu kwa kuhakikisha ya kuwa ninyi ni wana wake. Roho anayetuombea, akiita: “Baba!”


Kwa maana ninyi mumekufa na uzima wenu umefichwa pamoja na Kristo katika Mungu.


Basi wandugu zangu, muangalie vizuri, kati yenu kusikuwe mutu mumoja mwenye moyo mubaya wa kutokuamini, aliyefikia hata kujitenga mbali na Mungu Mwenye Uzima.


Vilevile tunaamini ujumbe uliotangazwa na manabii. Ninyi munafanya vema mukishikamana nao. Ujumbe huo ni kama taa inayoangaza pahali pa giza, mpaka wakati wa mapambazuko na wakati nyota ya asubui itakapoangazia mioyo yenu.


Tukisema kwamba hatukutenda zambi, tunamugeuza Mungu kuwa mwongo, na ukweli wa neno lake si ndani yetu.


Mutu yeyote anayeamini kwamba Yesu ndiye Kristo, yeye ni mutoto wa Mungu; na kila mutu anayemupenda baba anamupenda mwana wake vilevile.


Yule nyoka akamukasirikia yule mwanamuke na kwenda kufanya vita na wazao wake wengine; ndio wale wanaoshika amri za Mungu na kufuata ukweli ulioshuhudiwa na Yesu Kristo.


“Mwenye kuwa na masikio, asikie vizuri vile Roho anavyoyaambia makanisa! “Yule atakayeshinda, nitamupa ile mana iliyofichwa. Na nitamupa vilevile jiwe dogo jeupe, na juu yake kumeandikwa jina jipya ambalo hakuna mutu yeyote anayelijua, isipokuwa tu yule anayelipewa.


akiwa na uwezo sawa ule uliopewa na Baba yangu. Na zaidi ya ile nitamupa nyota ya asubui.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ