Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




1 Yoane 4:7 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

7 Wapendwa wangu, tupendane, kwa maana upendo unatoka kwa Mungu. Kila mutu anayekuwa na upendo ni mutoto wa Mungu naye anamujua Mungu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




1 Yoane 4:7
25 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Ninawapa amri mupya: mupendane ninyi kwa ninyi. Kama mimi nilivyowapenda, nanyi mupendane vilevile.


Nao uzima wa milele ni kukujua wewe unayekuwa peke yako Mungu wa kweli na Yesu Kristo uliyemutuma.


Lakini yule anayemupenda Mungu, huyu anajulikana naye.


Yule Mungu aliyesema: “Mwangaza uangaze katika giza,” ndiye aliyeangaza ndani ya mioyo yetu, na kutuwezesha kufahamu utukufu wa Mungu unaongaa kwenye uso wa Kristo.


Lakini sasa munamujua Mungu, au afazali tuseme kwamba sasa munajulikana naye. Basi namna gani mumerudilia tena vitu vinavyotawala dunia, visivyokuwa na uwezo na vikosefu, mukitaka kuwa watumwa tena?


Lakini tunda la Roho ni upendo, furaha, amani, uvumilivu, wema, fazili, uaminifu,


Yawe, Mungu wenu, atawafanya ninyi na wazao wenu mukuwe na moyo wa utii kusudi mumupende yeye kwa moyo wenu wote na roho yenu, mupate kuishi.


Kwa maana Mungu hakutupatia sisi Roho wa kuogopa, lakini Roho anayetupatia nguvu, upendo na kujizuiza.


Ninyi mumekwisha kutakaswa kwa njia ya kutii neno la kweli kwa kuwapenda wandugu zenu pasipo unafiki. Basi mupendane kabisa, kwa moyo wenu wote.


Yule anayemupenda ndugu yake, anaishi katika mwangaza na ndani yake hamuna kitu kinachoweza kuangusha mwingine katika zambi.


Munajua kwamba Kristo ni mwenye haki, kwa hiyo munapaswa kujua vilevile kwamba kila mutu anayefuata haki ni mutoto wa Mungu.


Sisi tunatambua kwamba tunamujua Mungu ikiwa tunashika amri zake.


Mutu akijidai kwamba anamujua Mungu, lakini hashiki amri zake, yeye ni mwongo, nao ukweli hauko ndani yake.


Wapenzi, siwaandikii amri mupya, lakini ile ya zamani muliyoijua tangia mbele. Na amri hiyo ya zamani ni lile neno mulilosikia.


Kila mutu anayekuwa mutoto wa Mungu hafanyi zambi, kwa sababu neno la Mungu linakaa ndani yake; tena hawezi kufanya zambi, maana Mungu ni baba yake.


Wapendwa wangu, ikiwa Mungu alitupenda sisi namna ile, sisi vilevile tunapaswa kupendana.


Hakuna hata mutu aliyekwisha kumwona Mungu wakati wowote. Tukipendana sisi kwa sisi, Mungu anaungana nasi na upendo wake unakamilika ndani yetu.


Na sisi tumejua na kuamini upendo Mungu anaokuwa nao kwetu. Mungu ni upendo. Yule anayeishi katika upendo anaungana na Mungu, na Mungu anaungana naye.


Kama mutu akisema “Ninamupenda Mungu,” naye anamuchukia ndugu yake, yeye ni mwongo. Kwa maana yule asiyemupenda ndugu yake anayemwona, hawezi kumupenda Mungu asiyemwona.


Mutu asiyekuwa na upendo hamujui Mungu kwa maana Mungu ni upendo.


Mutu yeyote anayeamini kwamba Yesu ndiye Kristo, yeye ni mutoto wa Mungu; na kila mutu anayemupenda baba anamupenda mwana wake vilevile.


Na sasa Mama, ninakusihi: tupendane. Basi hii si amri mupya ninayokuandikia, lakini ni amri ile tuliyopokea tangu mwanzo.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ